Binadamu : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Nyongeza sanduku la uanapwa
Mstari 24:
Watu wote walioko leo hii ni [[spishi]] ileile na tofauti zinazoonekana kati ya maumbile yao katika sehemu mbalimbali za dunia ni kidogo tu.
 
Utafiti juu ya [[DNA]] umethibitisha kwamba binadamu wote wametokana na watu waliokuwepo [[Afrika]] Mashariki walau miaka 200,000 hivi iliyopita.
 
Kwa namna ya pekee, upimaji wa [[DNA ya mviringo]], ambayo kila mmoja anarithi kwa mama tu, unaonyeshaulionyesha kuwa binadamu wote waliopo duniani wanachanga mama mmoja aliyewahi kuishi miaka 130,000 hivi iliyopita.
 
Halafu upimaji wa [[kromosomu Y]], ambayo kila mwanamume anarithi kwa baba tu, umeonyeshaulionyesha kuwa wanaume wote waliopo duniani wanachanga baba mmoja aliyewahi kuishi walau miaka 70,000 hivi iliyopita, kidogo kabla ya watubaadhi waya watu kwanzakuanza kuhama bara la Afrika na kuenea [[Asia]] labda kufuatia pwani za [[Bahari ya Hindi]].
 
Hata hivyo, miaka hii ya mwisho imegundulika katika baadhi ya wanaume wenyawenye asili ya kabila la [[Wambo]] ([[Camerun]]) aina ya kromosomu Y tofauti sana na ile ya wanaume wengine wote waliowahi kupimwa, kiasi cha kukadiria imetofautiana miaka 350,000 hivi iliyopita.
 
Vilevile, upimaji wa [[DNA ya mstari]] kwa jumla umeonyesha uwezekano wa kwamba baadhi ya binadamu wa leo, wale wasio wa kusini kwa [[Sahara]], wana asilimia 1-6 ya urithi wa kibiolojia kutoka kwa aina nyingine za homo, hususan [[Homo neanderthalensis]] na ile ya [[pango la Denisova]].
 
Kama hao waliweza kweli kuzaliana na [[Homo sapiens]] maana yake walikuwa [[spishi]] moja na yeye. Hapo asili ya binadamu inatakiwa kuhesabiwa ya zamani zaidi sana kuliko miaka 200,000.