Isotopi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
d Bot: Migrating 87 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q25276 (translate me) |
No edit summary |
||
Mstari 1:
'''Isotopi''' ni aina tofauti za [[atomi]] za [[elementi za kikemia]]. Isotopi za elementi fulani zina nambari sawa ya [[protoni]] katika [[kiini (atomi)|viini]] vyao lakini nambari tofauti za [[neutroni]].
Atomi ya elementi ya kikemia inaweza kupatikana kwa hali tofauti. Hali hizi tofauti huitwa isotopi.
Atomi zote za elementi moja ziko sawa katika
* idadi ya protoni kwenye [[kiini cha atomi]] na
* idadi ya elektroni kwenye [[mizingo elektroni]].
Isotopi za elementi moja zinatofautiana katika
*idadi ya [[nyutroni]] kwenye kiini cha atomi
*masi ya atomi yaani kiasi cha maada kilichopo ndani ya atomi.
Hali ya isotopi haibadilishi tabia za elementi na hapo ni asili ya jina "iso-topi" kutoka Kigiriki ''isos'' (ἴσος "sawa") na ''topos'' (τόπος "mahali"). Maana yake hata kama atomi hizi zina tabia tofauti za ndani zinapangwa mahali palepale kwenye [[jedwali la elementi]]. Ilhali tabia za nje za atomi zinatawaliwa na idadi ya elektroni katika mizingo elektroni, isotopi hazionyeshi tofauti ki[[kemia]] lakini kwa macho ya [[fizikia]] zinaweza kuwa tofauti.
Isotopi zinaweza kutofautishwa kwa makundi mawili:
*isotopi thabiti zinazokaa vilevile
*isotopi nururifu zinazoweza kubadilika
Elementi zote zinajulikana kuwa na isotopi, kuanzia moja hadi nyingi.
{{mbegu-kemia}}
[[Jamii:Kemia]]
[[jamii:fizikia]]
|