Nge : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
d →‎Picha: All info is kept in Wikidata, removed: {{Link FA|de}} using AWB (10903)
No edit summary
Mstari 19:
*[[Scorpionoidea]]
}}
'''Nge''' au '''akrabu''' (kutoka [[Kiarabu]] [[:ar:عقرب|عقرب]]) ni [[arithropodi]] wa [[oda]] [[Scorpiones]] katika ngeli [[Arakinida|Arachnida]]. Spishi ndogo huitwa '''visusuli''' pia. Kama arakinida wote wana [[mguu|miguu]] minane. [[Pedipalpi]] zao ni kubwa na zina gando, na mkia ni mrefu na una msumari mkubwa mwishoni kwake. Kama kawaida kiwiliwili chao kina sehemu mbili: [[kefalotoraksi]] ( [[w:cephalothorax|cephalothorax]]: [[kichwa]] na [[kidari]]) na [[fumbatio]] lakini zimeungwa vipana, siyo kwa [[pediseli]] ([[w:pedicel|pedicel]]) nyembamba kwa umbo wa mrija kama kwa [[buibui (Arithropodi)|buibui]]. Mgongo wa kefalotoraksi ni ngumumgumu na kwa hivyo huitwa [[gamba]] ([[w:Carapace|carapace]]). Nge wana [[jicho|macho]] 6-12, mawili juu ya gamba la kefalotoraksi na 2-5 kwa kila upande wa kichwa. Msumari wa nge hutumika kwa kudunga windo na kuingiza [[sumu]] ndani yake. Windo akiwa amekufa, [[kelisera]] ([[w:chelicera|chelicerae]]) za nge zinakata vipande vidogo vinavyowekwa katika kishimo mbele ya mdomo. Maji ya umeng'enyaji yakamuliwa katika kishimo hiki na baada ya kumeng'enya chakula myeyuko ufyondwa. Nge hula arithropodi wengine na wale wakubwa hula [[mjusi|mijusi]] na [[kipanya|vipanya]] wadogo pia.
 
== Picha ==