Mbu : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
dNo edit summary |
Sahihisho |
||
Mstari 23:
'''Mbu''' ni [[wadudu]] wadogo wa [[nusuoda]] [[Nematocera]] katika [[oda]] [[Diptera]] (yaani “wenye [[bawa|mabawa]] mawili”). Kwa asili jina hili limetumika kwa wadudu wa [[familia (biolojia)|familia]] [[Culicidae]], lakini kwa sababu [[spishi]] nyingi za Nematocera hazina majina ya [[Kiswahili]], “mbu” linapendekezwa kama jina kwa Nematocera wote. Nusuoda nyingine ya Diptera, [[Brachycera]], inashirikisha [[nzi]] na jamaa wao. Spishi ndogo za Nematocera huitwa usubi au [[kisubi (mdudu)|visubi]].
Diptera wote wana mabawa mawili tu yaliyopo kwa [[toraksi|mesotoraksi]]. Mabawa ya nyuma ya asili yamepunguzika na kubadilika kuwa [[rungu|virungu]] ([[w:Halteres|halteres]]) ambavyo vinasaidia mdudu ajue mkao wake na mabadiliko ya mwelekeo (kama aina ya [[gurudumu tuzi]]). Vipapasio vya Nematocera ni virefu kiasi na vina mapingili mengi kuliko Brachycera. Madume ya spishi nyingi zinabeba nywele nyingi juu ya vipapasio. Sehemu za kinywa za mbu
Spishi za mbu zinazojulikana sana ni zile ambazo hufyunza [[damu]]. Ni majike ambao wanafyunza damu, kwa sababu lazima wakuze [[yai|mayai]]. Madume na spishi nyingine za mbu hufyunza [[mbochi]] au utomvu. Mbu waladamu hurithisha [[ungonjwa|magonjwa]] mara nyingi, k.m. [[malaria]] (spishi za [[anofelesi]] (''[[Anopheles]]'')), [[homanyongo]], [[homa ya vipindi]], [[chikungunya]] (spishi za ''[[Aedes]]'') na [[matende]] (spishi za [[kuleksi]] (''[[Culex]]'')).
|