Ukristo : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Mstari 222:
 
Luther alitumia kwa nadra neno urekebisho, lakini likaja kuwa jina la kawaida la matukio yale mengi ya miaka [[1517]] - [[1555]], yaani kuanzia uenezi wa [[hoja 95]] za Martin Luther hadi [[amani ya Augsburg]]. Kati yake chanzo, yaani mabishano ya Kikanisa yaliyosababishwa na teolojia ya Luther, yalichanganyikana mapema na siasa, uchumi na utamaduni, kutokana na hali halisi ya wakati huo, mbali kuliko mwenyewe alivyofikiri.
 
Viongozi mbalimbali wakaiga mfano wa Luther, ila juhudi zao zikatofautiana: ndio mwanzo wa madhehebu mengine yanayoitwa ya "Kiinjili". Jina hilo linataka kusisitiza kwamba yanasimama kwenye msingi wa Injili tu, kinyume cha Kanisa Katoliki lililoona mapokeo yake kuwa na umuhimu pamoja na Biblia.
 
Kumbe wafuasi wa Luther na wengineo waliitwa na Wakatoliki "Waprotestanti", maana yake "wapinzani" (to protest = kupinga): neno hilo lilianza kutumika tangu wafuasi wa Luther walipopinga azimio la bunge lililotaka Wajerumani wote warudi chini ya Papa wa Roma.
 
Neno "Katoliki" tunaendelea kulitumia zaidi kwa maana ya madhehebu maalumu yenye wafuasi wengi duniani. Kiteolojia linamaanisha "Kanisa lililopo popote, lililo moja tu kila mahali na kila wakati". Kwa maana hiyo kila Mkristo yumo katika Ukatoliki, kwani mbele ya Kristo Kanisa ni moja tu, kila mahali duniani.
 
[[Waanglikana]], [[Walutheri]], [[Wamoravia]] na wengineo huamini kabisa kwamba wenyewe ni sehemu ya Kanisa lile moja la Bwana Yesu lililopo mahali popote.
 
Upande mwingine, hata Kanisa “Katoliki" linaloongozwa na Askofu (Papa) wa Roma ni la "Kiinjili" kwani linakubali na kutangaza Injili (= “habari njema”) ya Yesu Kristo.
 
Tangu mwaka [[1907]] tapo la [[Wapentekoste]] limeenea duniani kote (linakadiriwa kuwa na waumini milioni karibu 300) na kuathiri hata madhehebu yote ya zamani (ambapo mara nyingi waumini wa aina hiyo wanaitwa "[[Wakarismatiki]]").