Bamba la gandunia : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
jaribio la kutoa maelezo yanayoeleweka kirahisi zaidi
taipo
Mstari 1:
[[Image:Mabamba gandunia (tectonic plates).png|thumb|350px|Mabamba gandunia ya dunia yetu]]
'''Bamba gandunia''' ni jina kwa vipande vinavyofanya sehemu ya nje ya [[dunia]] yetu. Sehemu hii ya nje huitwa [[ganda la dunia]] na chini yake kuna sehemu ya dunia ambayo ni joto kiasi ya kwamba miamba na elementi zote zinapatikana katika hali ya giligili yaani kuyeyushwa. Hii sehemu ya nje ya dunia si kipande kimoja bali kuna vipande mbalimbali kandokando vinavyoelea juu ya mata ya moto ndani yake. Unaweza kusimakusoma zaidi katika makala kuhusu [[muundo wa dunia]].
 
Gandunia<ref>neno gandunia si kawaida bado, tunafuata hapo kamusi ya [[KAST]].</ref> ni elimu kuhusu ganda la dunia. Hoja la sayansi kuhusu [[gandunia]] ni ya kwamba ganda la dunia limevunjika kwa vipande mbalimbali vinavyoitwa mabamba. Kila bamba lapakana na mabamba mengine. Mabamba yasukumwa na mikondo ya moto chini yao kama majani yanayokaa usoni wa maji inayoanza kuchemka katika sufuria. Hivyo kila bamba lina mwendo wake wa pekee pamoja na au dhidi ya mabamba mengine. [[Tetemeko la ardhi]] ni dalili ya kwamba mabamba yamesuguana na hivyo kusababisha mishtuko tunayojua kama tetemeko la ardhi.