'''Sheikh Abeid Amani Karume''' alikuwa Rais wa kwanza wa [[Zanzibar]]. Alizaliwa mwaka [[1905]] na kufariki tarehe [[7 Aprili]] [[1972]] kwa kupigwa risasi.
Karume aliongoza mapinduzi yaliyomwangusha [[Sultani]] aliyekuwa akitawala Zanzibar hapo mwaka 1964. Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na [[Tanganyika (nchi)|Tanganyika]] iliyokuwa ikiongozwa na [[Mwalimu Nyerere]]. Baada ya muungano wa nchi hizi mbili uliozaa jina la [[Tanzania]], Karume alikuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
[[Amani Abeid Karume]], ambaye ni mtoto wa Sheikh Karume, ndiye rais wa sasa wa Zanzibar tangu mwaka 2000.