Klabu za Kiswahili : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika 'Yafuatayo ni baadhi ya malengo ya kuanzinshwa kwa klabu mbalimbali za Lugha ya Kiswahili katika shule mbalimbali za sekondari nchini Tanzania. <nowiki>*</nowik...'
(Hakuna tofauti)

Pitio la 13:06, 11 Septemba 2016

Yafuatayo ni baadhi ya malengo ya kuanzinshwa kwa klabu mbalimbali za Lugha ya Kiswahili katika shule mbalimbali za sekondari nchini Tanzania.

*1.Kukuza na kueneza Lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Tanzania.

*2.Kudumisha umoja na mshikamano kwa watumiaji wa Lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Tanzania.

*3.Kujifunza zaidi juu ya misamiati mipya ya Lugha ya Kiswahili baina ya watumiaji {Kupitia midahalo na majadiliano}.

*4.Kuibua wataalamu hodari wa kutumia Lugha ya Kiswahili kwa kuzingatia kanuni na taratibu za Lugha ya Kiswahili{sarufi ya Kiswahili},yaani katika kimatamshi,kimantiki na kimaana.

*5.Kuandaa wasanifishaji hodari wa Lugha ya Kiswahili au kufanya uwiano sawa wa kimatamshi katika Lugha.

*6.Kuibua vipaji mbalimbali vya sanaa mfano watunzi wa nyimbo{mashairi},ngonjera,hadithi{simulizi za kusisimua} na majigambo.Kwa lengo la kueneza tamaduni za Kiswahili{Mswahili}.

*7.Kuibua waandaaji hodari wa hotuba za Kiswahili ndani na nje ya nchi ya Tanzania kwa uzingatiaji wa kanuni,taratibu na sheria zote za uandaaji wa hotuba.

*8.Kuandaa wamahiri bora wa Lugha ya Kiswahili yaani wanaoweza kutumia Lugha ya Kiswahili katika nyanja kuu nne ambazo ni kusoma,kuandika,kusikiliza na kuzungumza kwa ufasaha.

*9.Kuandaa wakalimani hodari wa Lugha ya Kiswahili ambao watahamasisha wageni wengi kuwa na shauku ya kujifunza Lugha ya Kiswahili.

*10.Kuandaa watunzi bora wa kamusi za Kiswahili sanifu.