Bongo Flava : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
No edit summary
No edit summary
Tags: Mobile edit Mobile web edit
Mstari 20:
Jina la "bongo flava" ni tokeo la matini yaliyoharibiwa kutoka "bongo flavour", ambapo "bongo" ni wingi wa neno ''[[wikt:ubongo|ubongo]]'', ambapo mara nyingi huchukua nafasi ya kutaja jina la utani la [[Dar es Salaam]], jiji ambalo mtindo aina ya mtindo huu inatokea. Katika bongo flava, sitiari ya "bongo" inaweza kutaja zaidi maana ya ujanjaujanja wa mtaani, ya ''msela'' au masela wingi wake.<ref>{{cite journal|last=Stroeken|first=Koen|title=Immunizing Strategies: Hip-Hop and Critique in Tanzania|journal=[[Africa (journal)|Africa]]|volume=75|issue=4|pages=488–509|date=Winter 2005|doi=10.3366/afr.2005.75.4.488}}</ref>
 
Istilahi ya "bongo flava" ilitajwa kwa mara ya kwanza mnamo 1996 na Radio One 99.6 FM (moja kati ya redio za kwanza kabisa za binafsi nchini Tanzania) DR wa Redio [[Mike Mhagama]] ambaye alikuwa akijaribu kutofautisha kati ya muziki wa R & B na hip hop wa Marekani kupitia lipindi chake maarufu cha redio - 'DJ Show' ambapo enzi hizo vijana chipukizi walikuwa hawajaanza kutamba kwa mitindo yao wenyewe. DJ Show kilikuwa kipindi cha kwanza cha redio kukubali wanamuziki vijana wa Kitanzania wenye athira ya muziki wa Marekani - wakijieleza wenyewe kupitia uimbaji wa rap. Alisema hewani, "Baada ya kusikiliza kibao cha "R & B Flava" kilichoitwa 'No Diggity' kutoka Marekani, sasa inakuja "Bongo Flava" kutoka kwa [[Unique Sisters]], kutoka hapa nyumbani." Baada ya kusema hivyo katika kipindi, istilahi hii ya "Bongo Flava" ikanasa hadi leo hii.
 
Asili ya mwanzo kabisa na jinsi "Bongo flava" ilivyoanzishwa nchini Tanzania ni kutokana na [[Taji LuindiLiundi]] akiwa kama kiini cha hadithi hii. Kifupi hakuna asili bila yeye.
Taji Liundi pia anajulikana kama Master T, mwasisi, mwanzilishi na vilevile mtayarishaji wa kipindi cha Dj Show alishaanza kupiga nyimbo za wasanii wa ndani tangu mwishoni mwa miaka ya 1994. Mike Mhagama baadaye akajiunga na kipindi akiwa chini ya ukufunzi wa Master T. Aliendelea na kutangaza kipindi hicho peke yake hata baada ya Master T kuondoka Radio One mnamo 1996.
"Bongo flava" ilikaa vizuri sana hata kabla ya rekodi za video au sauti. Vijana mjini Dar es salaam walikuwa wakirap ufukweni mwa bahari kupitia matamasha mbalimbali (yameandaliwa na [[Joseph Kusaga]] ambaye anamiliki Mawingu Discothèque, baadaye Mawingu Studios na sasa ni [[Clouds Media Group]]), matamasha ya ndani yaliyochukua sura mpya rasmi baada ya kuanzisha mfululozo wa shindano la Yo!Rap Bonanza ambalo lilikuwa likichochewa na DJ Kim "And the Boyz" Magomelo.
Baadhi ya vijana walikuwa wakijipanga au kujiita majina ya kutunga au kundi fulani, baadhi yao walikuwa wakijitegemea au kujiweka katika kikundi fulani katika tukio hilo ilimradi wapate nafasi ya kukamata mic. Moja kati ya waliowahi kutamba katika mashindano ya kushika mic mwanzoni mwa miaka ya 1990 ni pamoja na Adili au Nigga One. Msanii maarufu wa kwanza wa mtindo huu aliyewahi kuiga ngoma za Marekani ni [[Saleh Jabir]] ambaye alirap kwa Kiswahili kupitia biti ya Vanilla Ice, "Ice Ice Baby", yeye ndiye aliyeanza kuweka Kiswahili katika rap. Toleo lake lilikuwa maarufu, ilivunja rekodi na kuweza kupigwa hata katika Redio ya Taifa la Tanzania. Ulikuwa wimbo wa kwanza wa rap ya Kiswahili kupaa anga ya Tanzania.
 
Moja kati ya makundi ya mwanzo kabisa kurekodi na kupeleka CD Radio One ili irushwe ilikuwa bendi ya Mawingu, kundi ambalo lilitamba sana mwanzoni mwa miaka ya 1994. Walirekodia katika Studio za Mawingu. Wanachama wake walikuwa kina Othman Njaidi, Eliudi Pemba, Columba Mwingira, Sindila Assey, Angela, Robert Chuwa, Boniface Kilosa (a.k.a. Dj Boni Love) na baadaye Pamela ambaye aliimba kibao chao kilichovunja rekodi cha RnB/Rap "[[Oya Msela]]". Wimbo ulikuwa maarufu mno na baadaye hilo neno likabaki hadi leo. Bendi ya Mawingu hujadilika kama waanzilishi wa ladha aina ya RnB ya Bongo flava.