Ulimwengu : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
Mstari 10:
Kwa maana hiyo dunia ni hasa sayari tunapoishi. Zamani watu waliona dunia kwa maana hiyo ni sawa na ulimwengu wote. Lakini maendeleo ya sayansi yametuonyesha upeo mkubwa zaidi uliopo ng'ambo ya sayari yetu na hata ng'ambo ya [[mfumo wa jua]] letu na sayari zake. Kwa hiyo neno "ulimwengu" limekuwa muhimu kwa sababu inalenga kiasili kwa jumla la vitu vyote si kwa sayari yetu hasa.
Katika wikipedia hii tunatumia neno "ulimwengu" kama [[Kiing.]] ''[[:en:universe|universe]]
Kwa Kiswahili ni afadhali kutofautisha vilevile. Kawaida tunatumia neno "anga" linalomaanisha kiasili kile kinachong'aa yaani mahali pa mwanga jinsi ilivyo anga juu yetu inayoangazwa na jua. Kutokana na maana haya ya kimsingi "anga" imemaanisha yote ambayo ni juu yetu. Hivyo "anga" inataja mara nyingi [[angahewa]] ya dunia, au yale buluu yanayoonekana juu yetu. Lakini hutumiwa pia kwa nafasi kubwa nje ya angahewa. Hapa tunatumia pia lugha ya "anga la nje" tukitaka kutofautisha angahewa na ile uwazi mkubwa kati ya sayari, nyota na galaksi.
|