Alfonso Maria Fusco

Alfonso Maria Fusco (Angri, Salerno, 23 Machi 1839 – Angri, 6 Februari 1910) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki huko Italia Kusini.

Alishughulikia hasa wakulima, akaanzisha shirika la kitawa la Masista wa Mt. Yohane Mbatizaji kwa ajili ya malezi ya vijana hasa fukara na yatima.

Alitangazwa mwenye heri na Papa Yohane Paulo II tarehe 7 Oktoba 2001, halafu mtakatifu na Papa Fransisko tarehe 16 Oktoba 2016.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.