Ali Kiba

Mwanamuziki wa Tanzania

Ali Salehe Kiba (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Ali Kiba; pia: King Kiba; alizaliwa mkoani Iringa, 26 Novemba 1986) ni mwanamuziki wa Tanzania, mwimbaji na mtunzi wa nyimbo chini ya lebo yake ya King's Music records na lebo aliyokuwa akiifanyia kazi Rockstar4000, ambayo alikuwa miongoni mwa wamiliki wake.

Ali Kiba

Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa Ali Salehe Kiba
Amezaliwa Novemba 29 1986 (1986-11-29) (umri 37)
Asili yake Iringa, Bendera ya Tanzania Tanzania
Aina ya muziki Mwanamuziki
Kazi yake Mwimbaji Mwanasoka
Aina ya sauti Sauti, piano
Miaka ya kazi 2006 hadi sasa
Studio Rockstars4000
Kings Music
Ame/Wameshirikiana na Aslay
Abdu Kiba
Christian Bella
Ommy Dimpoz
M.I
Patoranking
Abby Skills
Mr. Blue

Ana vipaji vilivyo tofauti na wasanii wenzake, hivyo amejikita sehemu nyingine kwa kusajiliwa na timu ya Mpira wa miguu Coastal Union ya mkoani Tanga kucheza mpira wa miguu kwa msimu wa 2018/2019 wa Vodacom Premier League.

Maisha hariri

Ali Kiba alizaliwa na Saleh Omari na Tombwe Njere. Ni mtoto wa kwanza kati ya watoto wanne kwenye familia yao, akifuatiwa na Abdu Saleh Kiba ambaye pia ni mwanamuziki, Zabib Kiba (dada yake) na Abuu Kiba (mdogo wao wa kiume wa mwisho).[1]

Mafanikio hariri

Mwaka 2011, Ali Kiba alichaguliwa kama msanii wa kwanza wa Afrika Mashariki - Tanzania, Kenya na Uganda.

Kwa mwaka 2015 ameshinda tuzo tano za Kilimanjaro Awards.

Tarehe 20 Mei 2016, kampuni ya kimataifa inayojishughulisha na muziki "Sony Music Entertainment" ilitangaza kumsainisha mkataba wa kufanya kazi na Ali Kiba.

Tuzo hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Himself Best International Act: Africa Ameshinda[2]

Nollywood and African Film Critics Awards hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Himself Favorite Artist Ameshinda
Mwana Favorite Song Ameshinda[3]

East Africa TV Awards hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Aje Best Male Artist Ameshinda
Song of the Year Ameshinda
Video of the Year Ameshinda

ASFA Awards (Uganda) hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Aje Most Stylish Artiste East Africa Ameshinda
Aje Most Fashionable Music Video Africa Ameshinda[3]

Soundcity Awards hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Aje Video of the Year Ameshinda

TZ INSTA Awards 2016 hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Aje Top Trending Song Ameshinda

Best Celebrity Player Awards (Uganda) hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Himself Best Celebrity Player Ameshinda

WANNAMusic Awards 2016 (France) hariri

Mwaka Kazi iliyoteuliwa Tuzo Matokeo
2016 Aje Best Male Artist Kigezo:Nominated
Best Collabo Kigezo:Nominated
People Choice Ameshinda

Tanbihi hariri

  1. https://globalpublishers.co.tz/historia-ya-maisha-ya-alikiba-tangu-kuzaliwa-video/
  2. "Ali Kiba atajwa kuwania Tuzo za MTV EMMA 2016". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 10 October 2016. Iliwekwa mnamo 7 October 2016.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); More than one of |archiveurl= na |archive-url= specified (help); More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help); More than one of |archivedate= na |archive-date= specified (help); Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  3. 3.0 3.1 "Annapita.com". www.annapita.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-10-09. Iliwekwa mnamo 2019-12-21. 

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ali Kiba kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.