Alpha Blondy (jina la kulizaliwa: Seydou Koné; * Dimbokoro, Côte d'Ivoire, 1 Januari 1953), ni mwanamuziki wa Reggae na msanii anayerekodi nyimbo zake nyingi kimataifa.

Seydou Koné
Mwanamzuki Alpha Blondy akitumbuiza.
Mwanamzuki Alpha Blondy akitumbuiza.
Jina Kamili {{{jina kamili}}}
Jina la kisanii Alpha Blondy
Nchi Ivory Coast
Alizaliwa 1953, Dimbokoro, Ivory Coast
Aina ya muziki Raggae
Kazi yake Muimbaji, Mtungaji
Miaka ya kazi 1982 - Mpaka leo
Ameshirikiana na Magic System
Ala Sauti

Alpha Blondy mara nyingi huimba kwa lugha ya Kidioula ambayo ndio lugha yake ya taifa huku akichanganya Kifaransa na Kiingereza, lakini pia wakati mwingine huimba kwa Kiarabu au Kiyahudi. Mashairi yake yanamaanisha siasa kali yenye mwelekeo na uchangamfu.

Maisha ya mwanzo hariri

Alpha ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto tisa, Jina la kuzaliwa ni Seydou Kone amezaliwa mjini Dimbokro mnamo 1953. Alilelewa na bibi yake mzaa mama. Mnamo mwaka 1962, Alpha Blondy alikwenda kukaa na baba yake aliyekuwa anaishi mjini Odienne, Ambapo alikaa kwa muda wa miaka kumi, Baadae akijiunga na shule ya Sainte Elisabeth high school, na kujishughulisha na makundi ya wanafunzi ya Ivory Coast. Hapo ndipo alipo unda bendi. Ingawaje, Upenzi huu uliathiri masomo yake na baadae Blondy alikufukuzwa shule kutokana na maudhulio mabovu shuleni.

Wazazi wake wakampeleka mtoto wao Alpha kusomea lugha ya Kiingereza mjini Monrovia, mji mkuu wa nchi jirani ya Liberia mnamo mwaka 1973. Huko alikaa kwa muda wa mwaka mmoja na mwezi mmoja kisha akamia nchini Marekani kwa kuongozea taaluma yake zaidi.

Alivyokuwa Marekani hariri

Mnamo mwaka 1973 Alpha amehamia mjini New York (Pia alishi kidoogo Texas), ni mahali alipomalizia chuo na aliegemea sana kwenye Kiingereza, Kwasabu toka mwanzo alikuwa anataka kuwa mwalimu wa lugha ya Kiingereza.

Alifanya kazi kwa juhudi zote,wakati mwingine hadi usiku, akitafuta hadi kuna kipindi anakuwa mgonjwa. Akiwa New York alikutana na Marastafari kwa mara ya kwanza, Pia alikuwa na uwezo wa kuangalia matamasha ya wanamuziki wa kijamaica kama kina Burning Spear n.k. Wakati huo yeye alikuwa akirekodi nyimbo za kikristo lakini hakuthubutu kuacha kuandika nyimbo zake mwenyewe.

Kwa bahti alikuwa akidodosa sehemu mabalimbali za mjini New York na baade kurudi kidoogo nichi Ivory Coast, Ambako alipata matatizo saana mpaka alivyokuja kukutana rafiki yake waliokuwa wote toka utoto, Fulgence Kassi, Ambaye baadae alikujua kuwa mtayarishaji maarufu wa vipindi vya television. Hapo ndipo alipoanza kuonekana kama kazi yake kweli ni uimbaji, na kutumia jina la 'Alpha Blondy'.

Imani yake hariri

Ana imani ya Kirasta (Rastafari)

Nyimbo maarufu hariri

Nyimbo ya kwanza kumpa mafanikio ilikuwa Brigadier Sabare. ni moja kati ya nyimbo zenye ujumbe:

  • Jah Glory - Hii aliimba juu ya upigaji vita umaskini.
  • Apartheid is Nazism
  • Brigadier Sabare - Nyimbo ilihusu ukatili wa maaskari.
  • Cocody Rock - Hii ilikuja kuwa ndio kama nyimbo yake ya taifa kila mtu anajua kuimba.
  • Guerre Civile - Hii ilihusu masuala ya vita ya wenyewe kwa wenyewe.
  • Jerusalem- Hii ilataka amani nchini israel. Nyimbo inaanza na maneno yanatumiwa katika sara za kiyahudi, Hivyo aliaza kiyahudi.
  • Journalistes en danger - Hii ilihusu mauaji ya Norbert Zongo aliyekuwa mchapishaji na mhriri wa gazeti la Independent la nchini Burkina Faso.
  • Politiqui - Hii ilihusu uraia.
  • Yitzhak Rabin

Albamu alizotoa hariri

  • 1982: Jah Glory
  • 1984: Cocody Rock!!!
  • 1985: Apartheid Is Nazism
  • 1986: Jerusalem (Alpha Blondy album)|Jerusalem (Akiwa na Wailers Band|The Wailers)
  • 1987: Revolution (Alpha Blondy album)|Revolution
  • 1989: The Prophets (album)|The Prophets
  • 1992: Masada (album)|Masada
  • 1993: SOS Guerres Tribales
  • 1993: Live Au Zénith (Paris)
  • 1994: Dieu
  • 1996: Grand Bassam Zion Rock
  • 1997: Best Of (Alpha Blondy album)|Best Of
  • 1998: Yitzhak Rabin (album)|Yitzhak Rabin
  • 1999: Elohim (Alpha Blondy album)|Elohim
  • 2001: Blondy Live Paris Bercy
  • 2002: Merci
  • 2005: "Akwaba"

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Alpha Blondy kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.