Anjela wa Msalaba (jina la awaliː María de los Ángeles[1] Guerrero y González, Sevilia, Hispania, 30 Januari 1846 - Sevilia 2 Machi 1932) alikuwa sista mwanzilishi wa shirika la Masista wa Msalaba ambalo ndani ya Kanisa Katoliki linahudumia mafukara na wagonjwa waliosahaulika kabisa.

Hakukubali kabisa kujipendelea kuliko hao akiwaita mabwana wake na kuwatumikia kabisa.

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 5 Novemba 1982 na mtakatifu tarehe 4 Mei 2003.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Ángela de la Cruz Guerrero González (1846–1932). Vatican New Service. Iliwekwa mnamo 2012-04-11.
  2. Martyrologium Romanum
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.