Bahari ya Timor (kwa Kiingereza: Timor Sea, kwa Kiindonesia: Laut Timor; kwa Kireno: Mar de Timor) ni bahari ya pembeni ya Bahari Hindi iliyopo baina ya kisiwa cha Timor na Australia. Eneo lake ni km2 61,500 na kimo chake hufikia hadi mita 3300 lakini wastani ni mita 406 pekee.

Ramani ya Bahari ya Timor mashariki mwa Bahari Hindi.

Eneo lake linapitiwa na mfereji wa Timor. Mkondo wa Indonesia unapita hapa ulio muhimu kwa sababu unabeba maji ya vuguvugu kutoka Pasifiki kwenda Bahari Hindi.

Kuna idadi ya visiwa na miamba matumbawe yasiyo na watu pamoja na vyanzo muhimu vya kabohidrati.

Tanbihi hariri

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

10°S 127°E / 10°S 127°E / -10; 127