Bahari ya Ufilipino

Bahari ya Ufilipino ni bahari ya pembeni ya Bahari Pasifiki iliyopo upande wa mashariki wa Ufilipino na Taiwan. Bahari ya Ufilipino imepakana na Japani upande wa kaskazini, Visiwa vya Mariana upande wa mashariki na Kisiwa cha Palau upande wa kusini. Eneo lake ni takribani kilomita za mraba milioni 5.

Bahari ya Ufilipino

Jiolojia hariri

Kijiolojia iko juu ya bamba la gandunia la Ufilipino. [1]

Mifereji mirefu zaidi duniani inapatikana katika eneo hilo ambayo ni Mfereji wa Mariana na Mfereji wa Ufilipino.

Marejeo hariri

  1. International Association for Earthquake Engineering. (2003). International Handbook of Earthquake and Engineering Seismology, Part 2, p. 1057.