Bahati (kutoka neno la Kifarsi/Kiajemi "bakht", بخت; pia: sudi; kwa Kiingereza: lucky) inatafsiriwa kwa namna tofauti.

Jani linalodhaniwa kuleta bahati njema.

Kwa mfano, Kamusi ya Noah Webster inafafanua bahati kama "nguvu isiyo na lengo, isiyotabirika na isiyotawalika inayosababisha matukio mazuri au mabaya kwa mtu binafsi au kundi la watu".[1]

Kumbe Max Gunther inatafsiri hivi: ni "matukio ambayo yanaathiri maisha ya mtu na yanaonekana kuwa nje ya udhibiti wake".[2]

Uwepo wa bahati unasadikiwa au kukanushwa kadiri ya utamaduni, falsafa, dini na hisia za watu. Kwa mfano Ukristo unafundisha Maongozi ya Mungu ambayo yanategemea Hekima yake, si bahati nasibu.

Tanbihi hariri

  1. Gunther, 1977. View on Google Books.
  2. Ibidem, Gunther, 1977.

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.