Baraza la maaskofu

Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Baraza la maaskofu (kwa Kiingereza Episcopal Conference) ni muundo wa Kanisa la Kilatini unaokutanisha maaskofu wa eneo fulani (kwa kawaida nchi huru fulani au nchi kadhaa, lakini pengine hata sehemu ya nchi kama hiyo ina maaskofu wengi sana).

Pengine ni wale tu wanaoongoza jimbo, pengine ni pamoja na waandamizi, wasaidizi au waliostaafu.

Pengine tena wanashiriki hata maaskofu wa eneo lile kutoka Makanisa Katoliki ya Mashariki.

Mabaraza ya namna hiyo zaidi ya 40 yalikuwepo kabla ya Mtaguso wa pili wa Vatikano ambao uliagiza yaanzishwe rasmi duniani kote (hati Christus Dominus, 38).

Kwa sasa yako 114, ambayo tena kwa kawaida yameunda mashirikisho ya kibara, kwa mfano "Symposium of Episcopal Conferences of Africa and Madagascar" (kifupisho: SECAM).

Pamoja na ustawi huo, teolojia haijafafanua vya kutosha mamlaka ya mabaraza hayo kuhusiana na ile inayoeleweka zaidi ya kila askofu katika jimbo lake na ya Papa wa Roma katika Kanisa Katoliki lote.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Baraza la maaskofu kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.