Betty Bayé

Mwandishi wa habari na mhariri wa Marekani

Betty Winston Bayé (alizaliwa Aprili 12, 1946) ni Mmarekani mwenye asili ya Afrika. Ni mwandishi wa habari, na mshiriki wa zamani wa bodi ya wahariri ya gazeti la Courier-Journal katika Louisville, Kentucky, na kampuni ya Gannett, ni mwenyeji wa kipindi cha "The Betty Baye Show". Yeye ni Makamu wa rais wa zamani wa Chama cha Kitaifa cha Wanahabari Weusi na ni maarufu sana.[1][2]

Betty Bayé
Jina la kuzaliwa Betty Winston Bayé
Nchi Marekani
Kazi yake Mwandishi wa habari
Watoto 3

Wasifu hariri

Betty Winston Bayé alilelewa, pamoja na dada zake wawili huko New York City, Harlem.[3][4] Wazazi wake walikuwa George na Betty Winston.[5] Bayé hakuenda chuo kikuu mara tu baada ya kumaliza shule ya upili. Alikuwa mfanyakazi kama karani na mwishoni mwa mwaka wa 1960 aliacha kazi iyo na kufwata ndoto yake ya kuwa mwigizaji katika ukumbi wa The National Black Theatre huko Harlem chini ya uongozi wa Barbara Ann Teer.[5][6] Mnamo 1979, Bayé alihitimu shahada ya kwanza ya Mawasiliano kutoka Chuo cha Hunter na mnamo 1980 shahada nyingine ya uandishi wa habari kutoka Chuo Kikuu cha The Columbia, Shule ya Uzamili ya Uandishi wa Habari. [7][5] [8]

Taaluma hariri

Bayé alikuwa na taaluma kadhaa wakati wa uhai wake. Alianza kufanya kazi ya ukarani kabla ya kwenda chuo kikuu.[3] Bayé alianza kazi yake ya utangazaji Mt. Vernon, New York for the Daily Argus from 1980–1984. Pia akawa mtangazaji wa Courier-Journal toka mwaka 1984–1986. Bayé alijiunga na bodi ya wahariri kama mhariri msaidizi kutoka mwaka 1986-1988 na kisha kuwa msaidizi wa mhariri wa majirani kutoka 1988-1990.[8] From 1990–1991, aliondoka Courier na kwenda kuwa mtu wa karibu wa Nieman huko Harvard. Alirudi kwenye kazi ya magazeti gazeti baada ya kuondoka huko Harvard.[7] Alifanya kazi uko "Courier" kwa karibu miaka thelathini na akaachishwa kazi na wafanyikazi wengine wengi wa Gannett.[9] Mbali na kazi yake ya magazeti, Bayé alichangia majarida kama "Essence Magazine", "Main Man", na "BlackAmericanWed.com".[1][7] Kwa miaka 6 alitangaza kipindi cha "The Betty Bayé Show" na pia alitangaza katika kipindi cha "Travis Smiley Show".[1][8]

Baadhi ya kazi zake za uandishi hariri

Bayé Aliandika vitabu viwili, "The Africans" Mwaka 1983 na "Blackbird" Mwaka 2000.[1][10] Bayé Alichangia kwenye kitabu cha "Family Affairs: What It Means to be African American Today",[8] "Tribe Became a Nation",[5] Na "Work Sister Work".[3] Pia alitajwa kwenye kitabu cha "Passing for Black: The Life and Careers of Mae Stret Kidd".[11]

Vitabu hariri

  • Betty Bayé, "Let's Talk Black", in Thinking Black: Some of the Nation's Best Black Columnists Speak Their Mind, edited by Dewayne Wikham. Crown Publishing Group, 1997.
  • Betty Bayé, Blackbird. Newport News, Va.: August Press, 2000.

Tuzo hariri

  • NABJ Hall of Fame 2013
  • Simmons College of Kentucky, honorary doctorate of humanities[10]

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 Betty Baye — Women's Center.
  2. Martin, Sunny C. (1 February 2007). Who's Who in Black Louisville: The Inaugural Edition. Who's Who Publishing Company. ISBN 9781933879161 – via Google Books. 
  3. 3.0 3.1 3.2 Shields, Cydney (2 February 1994). Work, Sister, Work: How Black Women Can Get Ahead in Today's Business Environment. Simon and Schuster. ISBN 9780671873059 – via Google Books. 
  4. Remembering Sgt. Clarence Lavon Floyd.
  5. 5.0 5.1 5.2 5.3 Dawkins, Wayne (18 October 1997). Black Journalists: The NABJ Story. August Press LLC. ISBN 9780963572042 – via Google Books. 
  6. Betty Baye: 'What's in a Name?'.
  7. 7.0 7.1 7.2 Riley, Sam G. (18 October 1995). Biographical Dictionary of American Newspaper Columnists. Greenwood Publishing Group. ISBN 9780313291920 – via Google Books. 
  8. 8.0 8.1 8.2 8.3 Robertson, Gil L. (18 October 2017). Family Affair: What It Means to be African American Today. Bolden. ISBN 9781932841350 – via Google Books. 
  9. Bailey, Phillip M. (1 December 2012). Noise and Notes: Betty Bayé (Still) Speaks! - 89.3 WFPL News Louisville.
  10. 10.0 10.1 About Betty Baye – Betty Baye Journalist.
  11. Hall, Wade H.; Hall, Wade; Kidd, Mae Street (25 November 1997). Passing for Black: The Life and Careers of Mae Street Kidd. University Press of Kentucky. ISBN 0813109485 – via Google Books.