Bodoni ni jina la fonti za serif zilizoundwa kwa mara ya kwanza na Giambattista Bodoni (1740-1813) mwishoni mwa karne ya 18 na ilitumiwa mara nyingi. Pia ni aina ya mwandiko unaopatikana kwenye kompyuta.

Bodoni

Aina za Bodoni zimeainishwa kama Didone au ya kisasa. Bodoni alifuata mawazo ya John Baskerville. Bodoni alikuwa na kazi ya muda mrefu na miundo yake ilibadilika na kuwa ya aina tofautitofauti.