Daniel Sturridge

Wachezaji mpira wa Uingereza

Daniel Andre Sturridge (alizaliwa mnamo 1 Septemba 1989) ni mchezaji wa soka wa Uingereza ambaye anachezea klabu ya Liverpool F.C. na timu ya taifa ya Uingereza. Anacheza kama mshambuliaji, lakini pia amekuwa akitumiwa kama winga wakati mwingine.

Daniel Sturridge akiwa Liverpool.

Alizaliwa Birmingham, Sturridge alitumia miaka minne katika chuo cha Aston Villa kabla ya kuhamia Coventry City. Kisha alijiunga na Manchester City mwaka 2003.

Aliendeleza maendeleo yake Manchester city na kucheza fainali mbili za FA Youth Cup. Aliifanya timu yake kuwa ya kwanza katika msimu wa 2007-2008.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Daniel Sturridge kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.