David wa Wales (kwa Kiwelisi 'Dewi Sant'; 500 hivi[1] - 589 hivi[2][3]) alikuwa mmonaki wa Welisi, halafu askofu wa Mynyw (sasa inaitwa St Davids kwa heshima yake).

Mt. David katika kioo cha rangi, Castell Coch, Cardiff.

Alitunga kanuni ya kimonaki kwa monasteri aliyoianzisha kwa kufuata mfano na desturi za mababu wa mashariki na alipinga vikali Upelaji. Wafuasi wake wengi waliinjilisha Welisi na nchi za kandokando (Ireland, Cornwall na Bretagne).[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na msimamizi wa Wales. Mwaka 1120 Papa Kalisti II alithibitisha heshima hiyo[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Machi[6].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1.   Toke, Leslie (1908). "St. David". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company.
  2. B text. Public Record Office, MS. E.164/1, p. 8. (Kilatini)
  3. Phillimore, Egerton (ed.), 1888 "The Annales Cambriae and Old Welsh Genealogies from Harleian MS. 3859", Y Cymmrodor; 9 (1888) pp. 141–183.
  4. http://www.santiebeati.it/dettaglio/43425
  5. Music for his Liturgy of the Hours has been edited by O. T. Edwards in Matins, Lauds and Vespers for St David's Day: the Medieval Office of the Welsh Patron Saint in National Library of Wales MS 20541 E (Cambridge, 1990).
  6. In the 2004 edition of the Roman Martyrology, David is listed under 1 March with the Latin name Dávus. He is recognised as bishop of Menevia in Wales who governed his monastery following the example of the Eastern Fathers. Through his leadership, many monks went forth to evangelise Wales, Ireland, Cornwall and Armorica (Brittany and surrounding provinces). Martyrologium Romanum, 2004, Vatican Press (Typis Vaticanis), page 171.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.