Eliodori wa Altino

Eliodori wa Altino (Dalmatia, leo nchini Korasya, katikati ya karne ya 4 - karibu na Venezia, Italia, 410 hivi) alikuwa askofu wa kwanza wa Altino kuanzia mwaka 380 hivi.

Panapotunzwa masalia yake.

Alikuwa mwanafunzi wa Valeriani wa Aquileia pamoja na Kromasi, halafu aliongozana na Jeromu kwenda Nchi Takatifu alipoishi kimonaki.

Aliporudi Italia alifanywa askofu (380 hivi), ila kidogo kabla ya kifo chake alikwenda kuishi upwekeni katika kisiwa kisicho na watu [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Julai[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Pio Paschini, Le vicende politiche e religiose del territorio friulano da Costantino a Carlo Magno (secc. IV-VIII), Memorie storiche forogiuliesi, Vol. 8, 1912, pag. 51-64.
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.