Epafrodito (kwa Kigiriki: Ἐπαφρόδιτος, yaani "Mpendevu"[1][2]) ni Mkristo wa karne ya 1 anayetajwa katika Agano Jipya[3] kama mjumbe wa kanisa la Filipi kwa kumhudumia Mtume Paulo kifungoni (Fil 2:25-30; pia 4:18). Akiwa huko aliugua, hivyo Paulo alipoona amepona akamrudisha Filipi kwa shukrani.

Epafrodito pamoja na Sosthene, Apolo, Kefa na Kaisari.

Paulo alimuita ndugu na mwenzi katika kazi na katika mapambano (ya utume).

Inasemekana baadaye akawa askofu.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 22 Machi[4] au 30 Machi[5].

Tanbihi hariri

  1. Bruce, Frederick F., 1989, Philippians, New International Biblical Commentary, New Testament Series, edited by W. Ward Gasque (Repr. Peabody, Mass.: Hendrickson, 2002), 99
  2. Joseph H. Thayer, C. L. Wilibald Grimm, and C. G. Wilke, 1889, Greek-English Lexicon of the New Testament (Repr. Grand Rapids, Mich.: Zondervan, 1966), 229.
  3. Monks of St. Augustine Abbey. "Epaphroditus (St.), The Book of Saints, A&C Black Ltd., London, 1921
  4. Martyrologium Romanum
  5. "Apostle Epaphroditus of the Seventy", Orthodox Church in America

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Epafrodito kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.