Farakano la mwaka 1054

Farakano la mwaka 1054 lilitokea hasa kati ya Papa Leo IX wa Roma na Patriarki Mikaeli Serulari wa Konstantinopoli likasababisha ushirika kati ya Ukristo wa Magharibi na sehemu kubwa ya Ukristo wa Mashariki usiendelee kuwa kamili hadi leo.

Hagia Sophia, kanisa kuu la Konstantinopoli wakati wa farakano.

Mahusiano yalikuwa yamezidi kuharibika tangu karne ya 4 ambapo ulianza ushindani kati ya miji hiyo miwili iliyokuwa kwa pamoja makao makuu ya Dola la Roma.

Maelekeo tofauti katika teolojia, maisha ya kiroho n.k. yalitumika kama visingizio katika kulaumiana, na hata kufarakana kwa muda.[1][2][3][4][5]

Hatimaye mabalozi waliotumwa na Papa, ingawa hawakuwa na mamlaka hiyo, waliacha juu ya altare ya kanisa kuu la Konstantinopoli hati ya kumtenga Patriarki na Kanisa Katoliki, naye akaitikia kwa kumtenga Papa na Kanisa la Orthodoksi.

Juhudi mbalimbali za kurudisha umoja zilifanyika katika nafasi mbalimbali, lakini pengine haraka haikusaidia kuzifanikisha, kwa mfano katika Mtaguso wa pili wa Lyon (1274) na katika Mtaguso wa Firenze (1431-1449).

Njia ya taratibu iliyoshikwa pamoja katika karne ya 20 inatia tumaini zaidi. Inakumbukwa hasa tamko la upendo la tarehe 7 Desemba 1965 ambalo Papa Paulo VI na Patriarki Atenagora I kwa pamoja walifuta kutoka kumbukumbu ya Kanisa hati za mwaka 1054 ambazo pande hizo mbili zilitengana.

Tanbihi hariri

  1. Cross, FL, mhariri (2005). "Great Schism (1)". The Oxford Dictionary of the Christian Church (article). New York: Oxford University Press. ISBN 0-19-280290-9. 
  2. D'Agostino, MG (2008), Il Primato della Sede di Roma in Leone IX (1049–1054). Studio dei testi latini nella controversia greco-romana nel periodo pregregoriano [The primacy of the Roman see in Leo IX (1049–54). Study of the Latin texts in the Greek-Roman controversy in the pre-Gregorian period], Cinisello Balsamo: San Paolo .
  3. Bayer, Axel (2002), Spaltung der Christenheit. Das sogennante Morgenländische Schisma von 1054 (kwa German), Köln-Weimar-Wien .
  4. Hergenröther, J (1869), Monumenta Graeca ad Photium eiusque historiam pertinentiam (kwa Latin), Regensburg, ku. 62–71 .
  5. Beck, Hans-Georg (1982), Byzantinisches Lesebuch (kwa German), München, ku. 245–47 .

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Farakano la mwaka 1054 kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.