Gallus Steiger (Bueron, Uswisi, 29 Machi 1879Peramiho, Songea, Tanzania, 26 Novemba 1966) alikuwa mmisionari, abate na askofu wa Kanisa Katoliki.

Kanisa la Wabenedikto huko Peramiho (2012), Gallus Steiger alipozikwa.

Maisha hariri

Alisoma katika shule maarufu ya abasia ya Wabenedikto huko Einsiedeln, Uswisi.

Mwaka 1902 alifunga nadhiri za utawa kama Mbenedikto huko St.Ottilien (Ujerumani).

Alitumwa kama mmisionari na kufika Dar es Salaam tarehe 4 Juni 1906.

Baada ya Waingereza kushinda Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, waliwafukuza wamisionari wenzake Wajerumani, lakini yeye kama raia wa Uswisi hakufukuzwa. Mwaka 1920 aliruhusiwa kuendelea na umisionari huko Ndanda kusini mashariki mwa Tanganyika. Mwaka 1922 aliteuliwa kuwa Prefect Apostolic wa huko Lindi akawa mkuu wa wamisionari Wabenedikto.

Mwaka 1928 alikuwa Abate (mwanzoni wa Lindi na mwaka 1931 Abate wa Peramiho) na aliwekwa wakfu kuwa askofu mwaka 1934 huko Einsiedeln.

Alistaafu mwaka 1953 akaendelea na umisionari hadi kufariki kwake huko Peramiho. Alizikwa kwenye kanisa kuu la Peramiho.

Marejeo hariri

  • Pugu Hadi Peramiho - kimehaririwa na P. Gerold Rupper, OSB, BPNP, Peramiho 1988, ISBN 9967 67 031 1

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.