Gereza

Sehemu ambayo watu wanaweza kufungwa kama sehemu ya kutumikia adhabu

Gereza (pia: jela kutoka Kiingereza: jail au prison) ni mahali ambako watu wanalazimishwa kukaa wakishikwa kinyume cha matakwa yao.

Gereza kwenye jimbo la New York, Marekani.

Kwa kawaida hali ya kufungwa ndani ya gereza ni adhabu iliyotolewa na mahakama kwa mtu aliyevunja sheria. Mara nyingi watu hufungwa ndani pia wakishtakiwa tu kuvunja sheria wakisubiri kesi zao zisikiwe mahakamani.

Katika nchi kadhaa serikali inatumia gereza kufunga watu wanaopinga viongozi wa nchi au kukosoa serikali.

Etimolojia hariri

Asili ya neno la Kiswahili "gereza" ni Kireno "igreja" inayomaanisha "kanisa" (la Kikristo). Maana imebadilika kwa sababu makanisa ya kwanza ya Wareno katika Afrika ya Mashariki yalijengwa ndani ya maboma yao. Kwa hiyo ilhali "igreja" ya Wareno ilikuwa ndani ya jengo imara ya ngome ilitokea kwamba ngome yenyewe ikaitwa hivyo. Hapo neno jipya "gereza" lilikuwa na maana ya "boma, ngome". Baadaye ngome hizo hazikuwa tena na kazi ya kijeshi kutokana na maendeleo ya teknolojia ya silaha, hivyo zilitumiwa kama jela kutunza wafungwa. [1]

Neno "jela" limekopwa kutoka Kiingereza "jail" wakati wa ukoloni wa Kiingereza.

Majengo hariri

 
Chumba cha mfungwa huko Montana, Marekani.

Gereza kimsingi ni jengo linalolindwa na lenye kuta nene, milango imara na madirisha yenye nondo zinazozuia kupita. Mara nyingi gereza huwa na majengo mbalimbali katika eneo kubwa lililoviringishwa kwa ukuta au fensi ya miiba. Nyumba za wafungwa ziko pamoja na ofisi za walinzi, mara nyingi pia karakana ambako wafungwa wanafanya kazi, nyumba ya jikoni na mengine. Minara inakaliwa na walinzi.

Vyumba vya wafungwa ni tofauti kati ya gereza na gereza; kuna vyumba ambako wafungwa wengi hushikwa pamoja; kuna vyumba vya wafungwa wawili-wawili. Nchi zinazofuata haki za binadamu hulenga kumpa kila mfungwa chumba chake cha pekee akiwa na nafasi ya kukutana na wafungwa wengine, kama kazini, wakati wa chakula au kwenye vipindi vya michezo. Kumtenga kabisa mfungwa na wafungwa wengine ni adhabu ya nyongeza.

Marejeo hariri

  1. "Etymologically speaking, the Kiswahili word gereza (prison) comes from the Portuguese igreja meaning church. This semantic change can be attributed to hostility greeted on the Portuguese by the then Islamised coastal communities forcing them to build their churches within the precincts of the fortresses." Adika Stanley Kevogo & Alex Umbima Kevogo: Swahili Military Terminology: A Case of an Evolving NonInstitutionalized Language Standard, Research on Humanities and Social Sciences ISSN (Paper) 2224-5766, ISSN (Online) 2225-0484 Vol.4, No.21, 2014, imeangaliwa kupitia https://www.researchgate.net/publication/325157378
  Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Gereza kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.