Hali ya hatari ni hali ambayo ikitangazwa inawezesha serikali kufanya vitendo ambavyo kwa kawaida hairuhusiwi kufanya kisheria. Serikali inaweza kutangaza hali hiyo wakati wa maafa, machafuko ya kiraia au vita. Tangazo la hali ya hatari huwatahadharisha wananchi kubadilisha maisha yao ya kawaida na huruhusu vyombo vya dola kutekeleza mipango ya dharura. 

Hali ya hatari pia inaweza kutumika kama kisingizio cha kutupilia mbali uhuru na haki zilizotolewa na katiba. Utaratibu na uhalali wa kufanya hivyo hutofautiana kadiri ya nchi.

Katika baadhi ya nchi, ni kinyume cha sheria ya kurekebisha sheria ya hali ya hatari au katiba ya wakati wa hali ya hatari. Katika nchi nyingine kuna uhuru wa kubadilisha sheria yoyote au haki zilizotolewa na katiba wakati wowote bunge linapoamua kufanya hivyo.

Sheria kulingana na nchi hariri

Kenya hariri

Mwaka 1952, serikali ya kikoloni ya Kenya, ikiongozwa na Evelyn Baring, ilitangaza hali ya hatari baada ya Mau Mau kuanza vita dhidi ya Wazungu na Waafrika waliowaunga mkono. Hali hiyo ilikwisha mwaka 1960 tu[1][2].

Katiba ya Kenya inakubali hali ya hatari wakati wa maafa asilia, vita, machafuko ya kisiasa au hali nyingine yoyote inayohitaji hali hiyo itangazwe. Rais atatangaza wiki mbili za hali ya hatari baada ya kupitishwa kwa azimio na wabunge thuluthi mbili. Kuongeza muda wa hali hiyo kunahitaji azimio lipitishwe na wabunge robo tatu. Hata hivyo, katiba inaruhusu mahakama ya juu kutupilia mbali azimio na sheria yoyote itakayopitishwa katika hali ya hatari. Haki za binadamu hazifai kukiukwa kwa muda ambao hali ya hatari itakuwepo[3].

Uhabeshi hariri

Hali ya hatari katika nchi ya Uhabeshi ilitangazwa Oktoba mwaka 2016 na aliyekuwa waziri mkuu, Hailemariam Desalegn, baada ya Waoromo kuandamana[4]. Sheria ya hali ya hatari iliwataka wanadiplomasia kutosafiri zaidi ya km 40 kutoka Addis Ababa, na kutokuwa na mawasiliano na vikundi vilivyosemwa kuwa magaidi. Pia, sheria hiyo ilipiga marufuku mikutano ya hadhara na kuwapa majeshi ya usalama nguvu za kuwatia ndani waliokiuka sheria hiyo bila idhini ya mahakama[5][4]. Ilikatizwa Agosti mwaka 2017.

Hali ya hatari ilitangazwa tena Februari mwaka 2018 kwa miezi sita, siku moja baada ya Hailemariam Desalegn kujiuzulu[6][7]. Juni mwaka 2018 bunge lilipiga kura kuikatiza hali ya hatari[8].

Marejeo hariri

  1. Leander (2013-11-07), "The longest state of emergency in Kenya ends", South African History Online (kwa Kiingereza), iliwekwa mnamo 2018-08-05 
  2. Ian Edgar Aplin (2014-06-12). "State of Emergency in Kenya, 1952-1960". Ian Edgar Aplin. Iliwekwa mnamo 2018-08-05. 
  3. "58. State of emergency - Kenya Law Reform Commission (KLRC)". www.klrc.go.ke (kwa en-gb). Iliwekwa mnamo 2018-08-05. 
  4. 4.0 4.1 "Legal Analysis of Ethiopia’s State of Emergency", Human Rights Watch (kwa Kiingereza), 2016-10-30, iliwekwa mnamo 2018-08-05 
  5. Deutsche Welle (www.dw.com). "Ethiopia regime unveils rules for state of emergency | DW | 16.10.2016". DW.COM (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2018-08-05. 
  6. Deutsche Welle (www.dw.com). "Sheria ya hali ya hatari Ethiopia na Migodi Magazetini | DW | 23.02.2018". DW.COM (kwa Kiswahili). Iliwekwa mnamo 2018-08-05. 
  7. "Hali ya hatari nchini Ethiopia kudumu kwa miezi sita ijayo – Taifa Leo". taifaleo.nation.co.ke (kwa Kiswahili). Iliwekwa mnamo 2018-08-05. [dead link]
  8. "Ethiopia lifts state of emergency", Daily Nation (kwa en-UK), iliwekwa mnamo 2018-08-05 
  Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Hali ya hatari kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.