Halima James Mdee

Mbunge wa Tanzania

Halima James Mdee (alizaliwa Makanya, Wilaya ya Same, mkoa wa Kilimanjaro, 18 Machi 1978) ni mbunge wa viti maalumu katika bunge la Tanzania, lakini si tena kupitia chama pinzani cha CHADEMA.

Maisha hariri

Halima James Mdee ni mtoto wa mwisho katika familia ya Profesa James Mdee ambaye alikuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kikabila ni Mpare.

Mdee alizaliwa katika familia ya Wakristo na alibatizwa kwa kuitwa Theodosia, hata hivyo anatumia zaidi jina alilorithi kutoka kwa bibi yake mzaa baba, Halima. Ukoo wake ni waumini wa dini ya Kiislamu, isipokuwa baba yake na kaka yake ambao walibatizwa na familia yao ikaridhia wawe Wakatoliki.

Elimu hariri

Alianza kusoma elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Mlimani jijini Dar es Salaam mwaka 1985 na kuhitimu mwaka 1991. Alichaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Wasichana Zanaki mwaka 1992 na kuhitimu kidato cha nne mwaka 1995.

Mwaka 1996 hadi 1998 alisoma kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kilakala mkoani Morogoro na 1999 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako alisomea sheria na kuhitimu mwaka 2003. Aliendelea kusoma shahada ya uzamili ya sheria katika chuo kikuu cha Pretoria (Afrika Kusini) [1] mwaka 2006 hadi 2007. [2]

Kazi na siasa hariri

Alipata ajira katika Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana mwaka 2004 akiwa Ofisa Maendeleo kama mwanasheria mpaka mwaka 2005 alipoamua kuacha kazi na kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, ambako alishiriki kuwapigia kampeni wagombea mbalimbali wa CHADEMA kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa viti maalumu.

Vyeo vya chama hariri

Mbali na ubunge, pia alikuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CHADEMA, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA na ofisa katika kurugenzi ya sheria.

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Halima James Mdee kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.