Hifadhi ya Taifa ya Amboseli

Hifadhi ya Taifa ya Amboseli, ambayo zamani ilikuwa inaitwa hifadhi ya wanyama ya Maasai Amboseli, iko katika Kaunti ya Kajiado (hapo awali tarafa ya Loitoktok, Wilaya ya Kajiado, Mkoa wa Bonde la Ufa), nchini Kenya.

Tembo wakitembea katika Hifadhi ya Taifa ya Amboseli National Park - Mlima Kilimanjaro unaonekana nyuma yao.
Tembo wakila katika madimbwi, kaskazini kwa Mlima Kilimanjaro.

Mbuga hii ina ukubwa wa hekta 39,206 au eneo la km2 392. Hifadhi ya Taifa ya Amboseli ni katika eneo linaloenea mpakani mwa Kenya na Tanzania.

Jina "Amboseli" linatokana na lugha ya Kimasai likimaanisha vumbi lenye ladha ya chumvi.

Wenyeji wa sehemu hii ni Wamasai, lakini watu kutoka maeneo mengine ya Kenya ni wakazi kutokana na mvuto wa kiuchumi. Uchumi wa Kajiado umenawiri kutokana na utalii wa wanaotembelea mbuga hiyo na kilimo kabambe kandokando ya mifumo ya mabwawa. Mabwawa hayo pia yanafanya eneo hili lenye mvua kidogo (wastani wa milimita 350 kwa mwaka) kuwa mojawapo ya sehemu bora duniani kuwatazama wanyamapori. Mbuga hiyo hulinda mabwawa mawili kwa matano ambayo yako, na inahusisha ziwa lililokauka la zamani za Pleistocene na mimea ya nusu-ukame.

Viungo vya njə hariri