Imani ya Kanisa (kwa Kilatini: fides Ecclesiae; kwa Kiingereza: Faith of the Church) ni wazo la msingi la teolojia ya Kanisa Katoliki. Maana yake ni kwamba imani si kazi ya Mkristo binafsi kwanza, bali ya Kanisa lote kwa pamoja[1].

Picha takatifu ya Mtaguso I wa Nisea, imani ya Kanisa ilipojitokeza dhidi ya uzushi wa Ario.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Kanisa ndilo lilipokea amana au hazina ya imani (depositum fidei) kwa Yesu Kristo kupitia Mitume wake. Likiongozwa na Roho Mtakatifu, alivyoahidi Yesu mwenyewe (Yoh 16:12-14), Kanisa linazidi kukumbuka na kuelewa yale yote yaliyofunuliwa naye, ili kwamba yawe hai karne hata karne.

Hata yakitokea mapungufu au kukosekana uwiano mzuri katika ufundishaji wa imani wakati fulani au katika eneo fulani, Kanisa zima linasadikika kuwa haliwezi kupotewa na ukweli, bali linazidi kuufahamu kikamilifu.

Vilevile, tendo la Mkristo kumsadiki Mungu na ufunuo wake linabebwa na imani ya taifa lake lote kama mtoto anavyobebwa na mama yake na kufundishwa naye kujua na kusema.

Hivyo Mkatoliki anahimizwa kushiriki zaidi na zaidi imani ya Kanisa lote (la nyakati zote na la mahali kote) ili azidi kusadiki kwa hakika, mbali na tafsiri binafsi zinazoweza kuathiriwa na umimi, na utamaduni n.k.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. This refers to the act of believing (fides qua creditur) as well as to the matters of doctrine (fides quae creditur)

Chanzo hariri