Ioni ni neno la fani ya kemia kwa ajili ya atomi au molekuli yenye chaji ya umeme.

Hali hii inatokea kama atomi au molekuli imepokea au kupotewa na elektroni kwa hiyo kuwa na ziada au upungufu wa elektroni kulingana na hali yake ya kawaida.

Sababu za atomi kuwa na chaji hasi au chanya hariri

Katika hali ya kawaida atomi haina chaji umeme kwa sababu ndani yake chaji tofauti zinajibatilisha yenyewe. Hii ni kweli pia kwa molekuli ambazo si kingine ila maungano ya atomi.

Atomi hujengwa na protoni, neutroni na elektroni. Protoni huwa na chaji umeme chanya, elektroni ni hasi na neutroni haina chaji.

Hali ya kawaida ya kila atomi ni uwiano sawa kati ya protoni (chanya) zinazofanya kiini cha atomi na elektroni (hasi) zinazozunguka kiini hicho.

 
Badiliko la atomi ya Natri kuwa kationi.

Njia zinazotumiwa na elektroni zikizunguka kiini huitwa mizingo elektroni. Mizingo elektroni hufuatana kama maganda ya kitunguu. Tabia ya kikemia ya elementi inategemea hali ya mzingo wa nje. Atomi ambayo mzingo wa nje una elektroni nane zimetosheleka, ziko katika hali thabiti yaani hazina hamu ya kupokea au kuachana na elektroni. Lakini nyingi huwa na idadi ndogo kuliko nane kwenye mzingo wa nje na kwa hiyo zinalenga kuingia katika hali thabiti ama kwa kuvuta elektroni kwao na kukamilisha nane au kuachana na elektroni ili kuondoa mzingo wa nje usio kamili.

Anioni na kationi hariri

Kwa hiyo ioni hutofautishwa katika aina mbili ambazo ni kationi na anioni.

Kationi ni ioni chanja yaani ni atomi / molekuli iliyotoa elektroni. Katika chombo cha elektrolisisi huvutiwa kwenye kathodi.

Anioni ni ioni hasi yaani atomi / molekuli iliyoongezwa elektroni. Katika chombo cha elektrolisisi huvutiwa kwenye anodi.

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ioni kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.