Isaka Mkuu (pia: Sahak Partev; 354 hivi - Bagrevand, 439) alikuwa mmonaki, mwanateolojia na askofu kutoka Armenia.

Mt. Isaka Mkuu alivyochorwa.

Mtoto wa Nerses I na kilembwekeza wa Gregori Mletamwanga, alipofiwa mke wake alijiunga na monasteri, halafu kama Patriarki alipigania umoja wa Kanisa kwa msingi wa imani sahihi ya Mtaguso wa Efeso.

Pia alisaidiana na Mesrop kutafsiri Biblia na alirekebisha liturujia na sheria za Kanisa[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Septemba[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/69620
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • (Kifaransa) Les dynasties de la Caucasie chrétienne de l’Antiquité jusqu’au XIXe siècle ; Tables généalogiques et chronologiques, Rome, 1990.
  • (Kifaransa) Histoire de l'Arménie: des origines à 1071, Paris, 1947.
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.