Ishmaeli (au Ismaili, kwa Kiebrania יִשְׁמָעֵאל, Yišmāʻēl: kwa Kiarabu إسماعيلʾ, Ismāʿīl) alikuwa mtoto wa kwanza wa Abrahamu (au Ibrahimu) na Hagari (au Hajiri) kadiri ya Biblia [1]na ya Kurani.

Agari na Ishmaeli jangwani kadiri ya François-Joseph Navez.

Ishmaeli katika Biblia hariri

Mungu alikuwa amemuahidia Abrahamu uzao mkubwa kama nyota za mbinguni, naye akaamini ingawa alikuwa hajapata hata mtoto mmoja: ndiyo imani iliyompendeza sana Mungu (Mwa 15:1-6).

Lakini Abrahamu alizidi kuzeeka pamoja na Sara bila ya kuzaa watoto. Baada ya kusubiri muda mrefu mno Sara akamwambia azaliane na Hagari aliye mtumishi wa kike. Mwana huyu wa Hagar akaitwa Ishmaeli (Mwa 16:1-15). Lakini baadaye kukawa na fitina kati ya Sara na Hagari hivyo huyo akafukuzwa pamoja na mtoto, baada ya Sara pia akashika mimba na kumzaa mtoto Isaka.

Mwa 21:1-21 inatusimulia jinsi Mungu alivyotimiza ahadi yake kwa kumjalia Sara amzalie Abrahamu mtoto huyo katika uzee na utasa. Isaka ni mtoto wa imani, si wa mwili, naye ni huru, tofauti na Ishmaeli mtoto wa mtumwa ambaye hastahili kurithi pamoja na mdogo wake. Isaka, baba wa Israeli alipata baraka kuu, naye ni mfano wetu watu wa Agano Jipya. Ishmaeli alibarikiwa pia kwa ajili ya baba yake, naye ni mfano wa Agano la Kale ambapo watu wanategemea mambo ya kimwili (kutahiriwa, kunawa, kubagua vyakula n.k.) na hivyo ni watumwa (Gal 4:21-5:1).

Kadiri ya kitabu cha Mwanzo alishiriki pamoja na mdogo wake Isaka mazishi ya baba yake akafariki akiwa na umri wa miaka 137.[2]

Ishmaeli alizaa watoto wa kiume 12 ambao wanahesabiwa mwanzo wa Waarabu, hasa wale wa Kaskazini.

Ishmaeli katika Uislamu hariri

 
Abrahamu akiwa tayari kumchinja Ishmael (upande wa juu wa mchoro mdogo wa karne ya 16 katika Zubdat Al-Tawarikh).

Ishmaeli anahesabiwa nabii muhimu na babu wa Muhammad, mwanzilishi wa dini ya Uislamu.

Ingawa Kurani haitaji jina la mtoto ambaye Abrahamu alikuwa tayari kumchinjia Mungu, wanazuoni walifikia makubaliano kwamba alikuwa Ishmaeli, si Isaka.

Tanbihi hariri

  1. Mwa 16:3
  2. Mwa 25:17

Marejeo hariri

Books and journals
Encyclopedias
  • Hubert Cancik, ed. (2005). Brill's New Pauly: Encyclopaedia of the Ancient World: Antiquity. Brill Academic Publishers. ISBN 978-90-04-12270-3
      .
  • Paul Lagasse, Lora Goldman, Archie Hobson, Susan R. Norton, ed. (2000). The Columbia Encyclopedia (6th ed.). Gale Group. ISBN 978-1-59339-236-9
      .
  • John Bowden, ed. (2005). Encyclopedia of Christianity (1st ed.). Oxford University Press. ISBN 0-19-522393-4
      .
      .
  • Lindsay Jones, ed. (2005). Encyclopedia of Religion (2nd ed.). MacMillan Reference Books. ISBN 978-0-02-865733-2
      .
  • The New Encyclopædia Britannica. Encyclopædia Britannica, Incorporated; Rev Ed edition. 2005. ISBN 978-1-59339-236-9
      .
      .

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ishmaeli kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.