Jinekomastia (en:gynecomastia kutoka Kigiriki γυνή, ginē = mwanamke na μαστός mastos = titi) ni tatizo la kiafya ambalo hukumba wanaume na kuwafanya waote matiti makubwa kuliko kawaida ya jinsia yao. Tatizo hili hutokea iwapo kuna shida ya mfumo wa vichocheo unaojulikana kwa Kiingereza kama estrogen-testosterone balance.

Mfano wa Jinekomastia kwa mtu mzima

Uwiano wa tesistosteroni na estrogeni hariri

Kwa mwanaume, homoni ya tesistosteroni inafaa kuwa kwa kiwango cha juu kuliko homoni ya estrojeni. Jinekomastia hutokea sanasana kwa watoto wachanga, wavulana wanapobalehe na pia kwa wazee wenye umri mkubwa.

Watoto wachanga huwa na matiti makubwa wawe wasichana au wavulana. Hili husababishwa na mvuko wa homoni ya estrojeni kutoka kwa mama mzazi hadi kwa mtoto alipo tumboni mwa mamaye. Hata hivyo, tatizo hili huisha baada ya wiki kadhaa anapozaliwa mtoto.

Wazee wanapovuka umri wa miaka arobaini kwenda juu hupawa na jinekomastia kwa sababu kiwango chao cha tesistosteroni kimepungua na kubatilishwa kuwa estrojeni. Mzee anapokuwa na shida kama hiyo hushauriwa aone daktari ili apewe mawaidha kuhusu steroidi anaboliki anazoweza kutumia ili kuongeza testosteroni.

Walioko katika hatari ya jinekomastia hariri

Tiba hariri

Wanywaji wa pombe huombwa kuacha tabia hiyo maana inawafanya wawe na tishu nyingi za mafuta mwilini. Pombe huwezesha mwili kuhifadhi mafuta kwa wingi.

Walio na unene wa kupindukia hushauriwa wafanye mazoezi kwa wingi na pia wale lishe bora isiyo na mafuta mengi. Mazoezi haswa ya kifua husaidia katika kuyeyusha ule ufuta ulioko kwa kifua.

Kwa wazee, tiba njema ni kuongezea homoni ya tesistosteroni mwilini kwa kutumia steroidi anaboliki.

Uchunguzi wa jinekomastia hariri

Jinekomastia yaweza kupimwa kwa njia zifuatazo:

1. Eksirei ya matiti. Hii hufanywa kuchunguza tishu za kawaida za matiti na kuzichanganua na zile zisizo za kawaida kama cysts, saratani na calcifications kwenye matiti.

2. Kipimo cha damu. Hicho hufanywa kuangalia wingi wa damu, chembechembe zilizoko na uwepo wa maambukizi ya bakteria.

3. Kipimo cha damu kuangalia wingi wa homoni ya tesistosteroni. Hicho hufanywa haswa asubuhi. Kiwango sawa cha homoni ya tesistosteroni huwa 300 hadi 1000 ng/dl. Hupungua kwa alama 13 wakati wa mchana.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  1. Sababu za wanaume kuota matiti
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jinekomastia kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.