Jorginho (alizaliwa tarehe 20 Desemba mwaka 1991) ni mchezaji wa Italia ambaye anacheza kama kiungo wa timu ya Chelsea F.C. na timu ya taifa ya Italia.

Jorginho akiwa Napoli.

Alizaliwa nchini Brazil, Jorginho alihamia Italia akiwa na umri wa miaka 15, na kuanza kazi yake ya kitaaluma na timu ya vijana wa Verona, kabla ya kukuzwa kwa timu kubwa. Wakati wa 2010-11, alipelekwa mkopo kwa Sambonifacese.

Mnamo Januari 2014, alihamia Napoli, ambako mara moja alishinda Coppa Italia na Supercoppa Italiana.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jorginho kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.