Kaunti ya Makueni ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Kaunti ya Makueni
Kaunti
Haven of Opportunities
Makueni County in Kenya.svg
Kaunti ya Makueni katika Kenya
Coordinates: 1°48′S 37°37′E / 1.800°S 37.617°E / -1.800; 37.617
Nchi Kenya
Namba17
IlianzishwaTarehe 4 Machi, 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Mashariki
Makao MakuuWote
Miji mingineEmali, Makindu, Kibwezi, Mtito Andei
GavanaProf. Kivutha Kibwana, EGH
Naibu wa GavanaAdelina Mwau Ndeto, OGW
SenetaMutula Kilonzo Junior
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa)Rose Mumo
Bunge la KauntiBunge la Kaunti ya Makueni
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa30
Maeneo bunge/Kaunti ndogo6
Eneokm2 8 169.8 (sq mi 3 154.4)
Idadi ya watu987,653
Wiani wa idadi ya watu121
Kanda mudaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovutimakueni.go.ke

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 987,653 katika eneo la km2 8,169.8, msongamano ukiwa hivyo wa watu 121 kwa kilometa mraba[1].

Makao makuu yako Wote.

Jiografia hariri

Kaunti ya Makueni imepakana na Machakos (kaskazini), Kitui (mashariki), Taita Taveta (kusini) na Kajiado (magaribi). Ni kaunti nusu kavu. Tabianchi hii huiwezesha Makueni kuzalisha maembe kwa muda mrefu kwa mwaka.

Mto Athi hupitia katika mpaka wa mashariki. Kulingana na utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta, asilimia 39 ya Makueni ina maji chini ya ardhi[2].

Tambarare ya Yatta huwa katika kaskazini mwa kaunti. Vilima vya Chyulu na Mbuga ya Kitaifa ya Vilima vya Chyulu huwa kusini mwa kaunti.

Utawala hariri

Kaunti ya Makueni imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo[3]:

Eneo bunge Kata
Mbooni Tulimani, Mbooni, Kithungo/Kitundu, Kiteta/Kisau, Waia-Kako, Kalawa
Kilome Kasikeu, Mukaa, Kiima Kiu/Kalanzoni
Kaiti Ukia, Kee, Kilungu, Ilima
Makueni Wote, Muvau/Kikuumini, Mavindini, Kitise/Kithuki, KathonzweniNzau/Kilili/Kalamba, Mbitini
Kibwezi West Makindu, Nguumo, Kikumbulyu North, Kimumbulyu South, Nguu/Masumba, Emali/Mulala
Kibwezi East Masongaleni, Mtito Andei, Thange, Ivingoni/Nzambani

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [4] hariri

  • Kathonzweni 79,780
  • Kibwezi 197,000
  • Kilungu 60,952
  • Makindu 84,946
  • Makueni 130,375
  • Mbooni East 97,756
  • Mbooni West 102,594
  • Mukaa 107,549
  • Nzaui 126,701

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30. 
  2. "Hope in Tapping Underground Water in Makueni - Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology". Iliwekwa mnamo 2018-04-26. 
  3. http://countytrak.infotrakresearch.com/Makueni-county/
  4. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.