Kiboko (Benin)

Lugha ya Mande nchini Benin na Nigeria

Kiboko ni lugha ya Kiniger-Kongo nchini Benin na Nigeria inayozungumzwa na Waboko. Isichanganywe na lugha ya Kiboko cha Kongo. Mwaka wa 1995 idadi ya wasemaji wa Kiboko nchini Benin imehesabiwa kuwa watu 70,000. Pia kuna wasemaji 40,000 nchini Nigeria. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiboko iko katika kundi la Kimande.

Majina hariri

Lugha ya Boko pia hujulikana kama Boko lakini pia hujulikana kama Boo au kwa jina la Hausa ni Busanci ( pia hutaandikwa Busanchi, Bussanci or Bussanchi)

Mtu mmoja au mzungumzaji mmoja wa lugha ya Boko huitwa Bokoni na watu wengi au wazungumzaji wengi huitwa Bokona. Lugha ya watu wa Bokona/Bussawa huitwa Bokonya.

Watu wa Boko ni mojawapo ya vikundi viwili vya watu wa Bissa, vingine vikiwa watu wa Busa, ambao wanazungumza lugha ya Busa. Wao si ukoo bali ni kikundi kidogo. Wao ni majirani wa watu wa Bariba, wanaozungumza lugha ya Bariba, ambayo ni lugha ya Gur. Watu wa Bissa wenyewe wanazungumza lugha ya Bissa, ambayo inafanana sana na Boko.

Mgawanyiko wa kijografia hariri

Nigeria hariri

Nchini Nigeria, lugha ya Boko inazungumzwa katika maeneo ya Borgu LGA ya Jimbo la Niger, Bagudo LGA ya Jimbo la Kebbi, na Baruten LGA ya Jimbo la Kwara. Baadhi ya watu wa Boko wamehamia sehemu nyingine za Nigeria, ikiwa ni pamoja na Abuja. Watu wa Boko wanaitwa Bussawa kwa lugha ya Hausa.

Benin hariri

Nchini Benin, lugha ya Boko inazungumzwa katika departimenti za Alibori na Borgou (Segbana na Kalalé Comunes).

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiboko (Benin) kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.