Kifulfulde-Adamawa

Kifulfulde-Adamawa ni lugha ya Kiniger-Kongo nchini Kamerun, Chad na Sudan inayozungumzwa na Wafulfulde. Lugha hiyo ni lugha mojawapo ya lugha za Kifulfulde. Mwaka wa 1986 idadi ya wasemaji wa Kifulfulde-Adamawa imehesabiwa kuwa watu 669,000 nchini Kamerun. Mwaka wa 1982 idadi ya wasemaji wa Kifulfulde-Adamawa imehesabiwa kuwa watu 90,000 nchini Sudan, na wachache wengine wako nchini Sudan Kusini. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kifulfulde-Adamawa imehesabiwa kuwa watu 148,000 nchini Chad. Pia kuna wasemaji nchini Nigeria na Marekani. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kifulfulde-Adamawa iko katika kundi la Kiatlantiki.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kifulfulde-Adamawa kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.