Kiraitu Murungi (alizaliwa 1 Januari 1952) ni mwanasiasa nchini Kenya. Alituhumiwa kuhusika katika kashfa ya Anglo leasing.

Kiraitu Murungi

Elimu hariri

Murungi alizaliwa mjini Meru. Yeye alisomea shule za Upili Chuka High School na Alliance High School, kisha akatoka katika Chuo Kikuu cha Nairobi na kufuzu kama shahada ya Sheria mwaka wa 1977 na kama Mwalimu wa Sheria mwaka wa 1982. Yeye baadaye akapata Uwalimu wa Sheria katika Chuo Cha Sheria Cha Harvard mwaka wa 1991.[1]

Wasifu katika Sheria hariri

Murungi alikuwa mshirika katika sheria imara iliyoanzishwa pamoja na Gibson Kuria Kamau. Kesi yake kubwa wakati huu ilikuwa ni kuwakilisha umiliki wa wafungwa wa kisiasa na serikali ya Moi pamoja naWanyiri Kihoro dhidi ya serikali yenyewe [2] Kesi ambayo inatajwa mara nyingi katika kitabu cha Wanyiri Kihoro "Never Say Die" "The Chronicle of a Political Prisoner" iliyosababisha kufungwa kwa Bwana Kuria kwa majaribio ya kuwacha kesi (0/), vilevile kipindi uhamishoni ya nchi za magharibi kwa Mr Murungi na Bw Kuria. {1/}

Wasifu wa kisiasa hariri

Murungi amekuwa Mbunge tangu mwaka wa 1992 na hapo awali aliwahi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na Mwanasheria Mkuu(wakilishi). Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka wa 2002 nchini Kenyaalishinda [[Kiti cha mbunge Imenti Kusini kutoka chama cha "National Rainbow Coalition"|Kiti cha mbunge Imenti Kusini kutoka chama cha "National Rainbow Coalition"]] (NARC). Baada ya serikali kushindwa katika mwaka wa 2005, 21 Novemba katika kura ya maoni kikatiba, aliteuliwa kuwa Waziri wa Kawi.

Katika mwaka wa 2005 Februari, Murungi aliomba msamaha kwa kutoa matamshi ambayo yaliyokaguliwa kuwa yanaenezaubakaji na rushwa. Yeye alikuwa amesema kuwa ukaguzi kutoka kwa wahisani wa misaada ya rushwa nchini Kenya ilikuwa "ni kama kubaka mwanamke ambaye ako tayari" [3]

Kashfa ya "Anglo Leasing" hariri

Yeye ni mmoja wa washirika wa karibu wa Rais wa Kenya Mwai Kibaki. Amekuwa akishutuhumiwa kwa majaribio ya kufunika katika kashfa ya "Anglo Leasing" , ambayo yeye alidai kuwa ni kashfa ambayo haikuwahi kuwa".[4]

Katika mwaka wa 2006, 8 FebruariShirika la Utangazaji la BBC ilitoa mazungumzo kati ya Mweshimiwa Murungi na Katibu wa zamani wa Utawala Bora na MaadiliBw.John Githongo ambapo inaonekana kuwa anajaribu kumwambia Bw. Githongo kuachana na uchunguzi wake juu ya kashfa ya "Anglo Leasing". Yeye aliahidi kwamba Anura Pereira atasamehe madeni ya KES milioni 30 ambazo zilikuwa zinadaiwa babake Githongo.[5]

Murungi awali alisisitiza kuwa kamwe hakutaka kujiuzulu kutoka kiti chake cha Waziri licha ya madai ya rushwa.[6] Yeye alidai kwamba hana hatia na kuwa ripoti ya Githongo ni propaganda tu. Juu ya kurekodi, yeye alitoa maoni ya kuwa: "Nimeyasikiliza madai ya kanda ya ushahidi. Ni njia ya mkato, haisikiki, haitoshi na haikubaliki kuunda ushahidi unaoaminika kwa madai yaliopangwa na Bw. Githongo " [7] Tarehe 13 Februari 2006, hata hivyo, Rais Mwai Kibaki alitangaza kuwa Murungi amejiuzulu kuruhusu uchunguzi kamili juu ya hayo madai [8] Tarehe 14 Februari 2006, siku baada yake kujiuzulu, Murungi alidai kuwa yeye hakuhusika kwa kufunika kashfa ya Anglo Leasing. Yeye alilaumu shida zilizomo kisiasa katika chama chaNational Rainbow Coalition (NARC) na vyombo vya habari. Hata hivyo, baadaye iliibuka kwamba Rais Mwai Kibaki alimuuliza ajiuzulu kutoka kwa Serikali.[9]

Tarehe 15 Novemba 2006 alirudishwa kazini kama Waziri wa Kawi na Rais Kibaki.[10] Yeye alibakia katika nafasi hiyo katika baraza la mawaziri walioteuliwa na Rais Kibaki Tarehe 8 Januari 2008 kufuatia utata wa uchaguzi wa Desemba 2007. [11]

Kamati ya Uchunguzi ya Hesabu Ya Bunge hariri

Tarehe 10 Februari 2006, Murungi alitoa taarifa ambayo ilichapishwa na kutumwa kwa vyombo vyote vya habari nchini Kenya ikihoji nia na madhumuni ya John Githongo, katika maswali thelathini na sita. Kati ya maswali ambayo aliuliza ni kwa nini John Githongo alikuwa ananasa mazungumzo yake na maafisa wa Serikali na kama alikuwa mpelelezi wa mataifa ya kigeni.[12]

Angalia Pia hariri

Viungo vya nje hariri

Marejeo hariri

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2006-03-07. Iliwekwa mnamo 2009-12-22.
  2. [1] ^ WANYIRI KIHORO vs Mwanasheria Mkuu [Mahakama ya Rufaa mjini NAIROBI (GACHUHI, MASIME & KWACH JJA) CIVIL APPEAL NO. 151 WA 1988 http://www.kituochakatiba.co.ug/wanyiri.htm
  3. "Kenyan apology over rape remark", BBC News, 11 Februari 2005. Retrieved on 2006-02-13. 
  4. "The Big Question: Can the President Shake Off Men in the Eye of a Storm?", The Daily Nation, 29 Januari 2006. Retrieved on 2006-02-13. 
  5. "'Taped evidence' in Kenya scandal", BBC News, 9 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-10. 
  6. "Kenyan minister 'not resigning'", BBC News, 10 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-10. 
  7. "Kiraitu: 'BBC Tape Not Credible'", Daily Nation, 10 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-10. 
  8. "Kenyan 'graft' ministers resign", BBC News, 13 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-13. 
  9. "Kibaki asked Kiraitu and Saitoti to quit", Daily Nation, 13 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-16. [dead link]
  10. [18] ^ Rais Kibaki anawarudisha mawaziri baada ya kashfa, IOL
  11. [4] ^ "Kenya: Rais Kibaki achagua baraza la Mawaziri", The East African Standard (allAfrica.com), 8 Januari 2008.
  12. "Minister Kiraitu’s 36 questions to Githongo", Standard, Kenya, 10 Februari 2006. Retrieved on 2006-02-13. Archived from the original on 2006-10-29.