Kiserbia ni tawi la Kiserbokroatia, moja kati ya lugha za Kislavoni, za jamii ya Lugha za Kihindi-Kiulaya, linalozungumzwa na watu milioni 8.5 - 9.5, zaidi katika nchi ya Serbia.

Kiserbia kilikuwa lugha rasmi ya Yugoslavia pamoja na Kislovenia, Kikroatia na Kimasedonia.

Kufuatana na tofauti za utamaduni na madhehebu, Kiserbokroatia kinaandikwa kwa alfabeti ya Kilatini upande wa Magharibi katika eneo la Kroatia na kwa alfabeti ya Kikirili upande wa Mashariki katika eneo la Serbia.

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiserbia kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.