Kitabu cha Habakuki

Habakuki ni jina la nabii wa Israeli ya Kale na pia la kitabu kinacholeta habari zake katika Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania), na kwa hiyo pia katika Agano la Kale, sehemu ya kwanza ya Biblia ya Kikristo.

Sanamu ya Habakuki iliyotengenezwa na Donatello, Museo dell'Opera del Duomo, Florence.

Muda na mada hariri

Wakati alipofanya kazi nabii Yeremia aliishi pia Habakuki (600 hivi K.K.), aliyeandika kitabu kifupi ambamo alithubutu kumuuliza Mungu kwa nini anaadhibu Israeli vikali kwa mikono ya watu wabaya kuliko wao.

Jibu ni kwamba Mwenyezi Mungu ana njia zake ambazo anaandaa ushindi wa haki: hivyo mwadilifu ataishi kwa imani yake (1:12-2:4).

Usemi huo ukaja kutumika sana katika Agano Jipya. Mtume Paulo ameufanya msingi wa msimamo wake kuwa wokovu unapatikana kwa imani, si kwa kujitahidi kutekeleza masharti yote ya Torati.

Ufafanuzi hariri

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Marejeo hariri

Viungo vya Nje hariri

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

  Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Habakuki kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.