Kumasi ni mji mkubwa wa pili nchini Ghana na mji mkuu wa Mkoa wa Ashanti.

Kumasi mjini

Tangu mwaka 1695 ilikuwa mji mkuu wa Ufalme wa Ashanti na Asantehene (mfalme wa Waashanti) anakalia hadi leo jumba lake mjini. Ndipo kilipo "kikalio cha dhahabu" cha Asantehene ambacho kinaaminiwa kimeteremshwa kutoka mbinguni.

Mwaka 2005 mji ulikuwa na wakazi 862.000. Umbali kutoka Accra ni km 250. Kuna Chuo Kikuu cha Kwame Nkrumah cha Sayansi na Teknolojia.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa UM Kofi Annan alizaliwa Kumasi.

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kumasi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.