Kwa maana nyingine ya jina hili angalia hapa

Kwale ni kisiwa kidogo katika Bahari Hindi mbele ya pwani ya Tanzania upande wa kaskazini wa delta ya mto Rufiji.

Kisiwa hicho ni sehemu ya kata ya Kisiju kwenye wilaya ya Mkuranga (Mkoa wa Pwani).

Kwale imetambuliwa na wataalamu wa akiolojia kuwa kati ya vituo vya awali vya biashara ya pwani iliyokuwa chanzo cha utamaduni wa Uswahilini. [1]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. [http://iodeweb1.vliz.be/odin/bitstream/1834/278/1/chami.pdf Early Iron Working People's Adaptation to the Nearshore and Offshore Island Environment by Felix Chami]

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Pwani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kwale (Kisiju) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.