Lango hili lipo katika ujenzi

Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia


Jambo!!!
Karibu (Welcome)

WikiLango Kenya

Flag of Kenya
Flag of Kenya
Coat of Arms of Kenya
Coat of Arms of Kenya
Location of Kenya

Jamhuri ya Kenya ni nchi iliyoko Afrika Mashariki katika ikweta, kando ya Bahari ya Hindi. Kenya imepakana na Ethiopia (kaskazini), Somalia (kaskazini mashariki), Tanzania (kusini), Uganda na Ziwa Victoria (magharibi), kisha Sudan Kusini (kaskazini magharibi). Mji mkuu ni Nairobi.

Mji mkuu ni Nairobi. Idadi ya watu imeongezeka katika miaka ya hivi karibuni na kufikia milioni 50. Kenya ina mbuga mbalimbali wanamoishi maelfu ya wanyama pori wa kila aina.

Jina Kenya linatokana na mlima Kenya, ulio wa pili kwa urefu barani Afrika, Kabla ya mwaka wa 1920, eneo linaloitwa Kenya liliitwa Himaya ya Uingereza Afrika Mashariki, kwa hivyo hapakuwa na haja kutaja neno mlima uliporejelea mlima huo.

Makala iliyochuguliwa

Nairobi

Nairobi ni mji mkuu wa Kenya na vilevile mmojawapo wa mikoa ya Kenya. Ni kati ya miji mikubwa ya Afrika. Kulingana na sensa ya 2009, Nairobi ina wakaaji 3,138,295. Pamoja na vitongoji vyake, Nairobi ni mji wa 12 kwa ukubwa barani Afrika.

Jina Nairobi limetokana na neno la Kimaasai, Enkare nairobi, linalomaanisha "mahali penye maji baridi." Lugha zote za Kenya huzungumzwa Nairobi, lakini hasa Kiingereza na Kiswahili, pamoja na Sheng. (Soma zaidi...)

Picha iliyochaguliwa

Giraffe in Nairobi
Giraffe in Nairobi
Twiga katika Hifadhi ya Nairobi ikiwa na mijengo na anga ya Nairobi nyuma yake.

Je wajua ...

  • ... kwamba wanafunzi katika nchi ya Kenya hufunzwa kwa lugha ya Kiingereza?
  • ... la kwamba jina rasmi la Kenya ni Jamhuri ya Kenya?
  • ... la kwamba Ziwa Turkana ndio ziwa kuu katika jangwa ulimwenguni?
  • ... kwamba Kenya ina upaka na 'ziwa kubwa kwa eneo ya Afrika, Ziwa Victoria' ?
  • ... kwamba Mlima Kenya ni mlima wa pili kwa urefu katika Afrika? Ni 5,199 metres (17,057 ft).
  • ... ya kwamba asilimia thelathini na tatu ya maua katika Umoja wa Ulaya hutoka Kenya?
  • Wasifu uliochaguliwa

    Mwai Kibaki ni rais wa tatu wa Jamhuri ya Kenya akiwa ametanguliwa na Rais wa Kwanza wa Kenya,Mzee Jomo Kenyatta, na Daniel Arap Moi. Jina lake la kubatizwa ni Emilio Stanley.

    Kibaki alisoma uchumi, historia na sayansi ya siasa katika chuo kikuu cha Makerere, Kampala, Uganda. Akiwa mwanafunzi Makerere, Kibaki alikuwa ni mwenyekiti wa chama cha wanafunzi toka Kenya, Kenya Students' Association. Alipomaliza masomo yake mwaka 1955 alipewa tuzo kutokana na kufanya vyema katika mitihani. Tuzo hiyo ilimwezesha kwenda kusoma katika chuo cha London School of Economics. Alipomaliza masomo alikwenda kufundisha katika chuo kikuu cha Makerere. Baadaye aliacha kazi ya kufundisha na kuwa mtendaji mkuu wa chama cha Kenya African National Union.

    (Soma Zaidi...)

    Jamii

    Masomo inayohusu Kenya

    Milango inayohusiana

    Associated Wikimedia

    Kenya on Wikibooks  Kenya on Wikimedia Commons Kenya on Wikinews  Kenya on Wikiquote  Kenya on Wikisource  Kenya on Wikiversity  Kenya on Wiktionary 
    Manuals and books Images and media News Quotations Texts Learning resources Definitions