Leif Erikson (pia Ericson, Erickson, au Ericksson, mnamo 970 - 1020 BK) alikuwa mpelelezi kutoka Skandinavia. [1] Alikuwa Mzungu wa kwanza anayejulikana kusafiri kwenda Amerika Kaskazini.

Stempu ya posta ya Visiwa vya Faroe Ugunduzi wa Amerika: Leif Erikson.
Stempu ya posta ya Marekani ya mwaka 1968.

Maisha hariri

Hakuna habari za uhakika juu yake. Uwezekano mkubwa ni kwamba Erikson alizaliwa huko Iceland. Baba yake alikuwa Erik Mwekundu, [1] hivyo mwanawe Leif aliitwa "Erikson" yaani mwana wa Erik. Erika Mzee alikuwa ameunda makoloni huko Greenland. Erikson anasemekana alitembelea Amerika Kaskazini muda mrefu kabla ya mtu yeyote kutoka Ulaya kufanya hivyo. Kulingana na masimulizi ya Iceland aliunda makazi ya Waviking huko "Vinland". Wasomi wengi wanadhani hii ilikuwa Newfoundland katika Kanada ya leo.

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 Leif Eriksson the Lucky. Encyclopædia Britannica. Iliwekwa mnamo 6 March 2011.

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Leif Erikson kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.