Loris Karius

Mchezaji wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini Ujerumani

Loris Sven Karius (alizaliwa 22 Juni 1993) ni mchezaji wa soka wa Ujerumani ambaye anacheza kama golikipa wa klabu ya Ligi Kuu ya Uingereza Liverpool F.C.. Aliwakilisha Ujerumani wakati wa michezo ya vijana.

Loris Karius akirukia mpira.

Alizaliwa huko Biberach, Karius alianza kazi yake na Stuttgart kabla ya kuhamia Manchester City mwaka 2009.

Baada ya miaka miwili katika mfumo wa vijana wa Manchester City, alirudi Ujerumani katika timu ya Mainz 05.

Baada ya miaka mitano Karius alihamia Liverpool mwaka 2016 kwa ada ya £ milioni 4.75.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Loris Karius kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.