Matamshi (kutoka kitenzi "kutamka") ni namna au jinsi watu wanasema hali halisi maneno ya lugha fulani, ambayo inaweza kuwa tofauti na namna ya kuandika neno. Utafiti wa utamshi au utamkaji ni kazi ya somo la fonetiki, tawi mojawapo la isimu.

Sehemu zinazohusika na matamshi.

Matamshi yanaweza kutofautiana kati ya eneo na eneo, na hata kati ya mtu na mtu kulingana na alikoishi utotoni, makazi yake ya sasa, shida katika kutoa sauti[1], kabila, dini, tabaka la kijamii, elimu[2] n.k.

Pengine tofauti hizo husababisha lahaja.

Tanbihi

  1. Beech, John R.; Harding, Leonora; Hilton-Jones, Diana (1993). "Assessment of Articulation and Phonology". Katika Grunwell, Pam. Assessment in Speech and Language Therapy. CUP Archive. uk. 55. ISBN 0-415-07882-2. 
  2. Paulston, Christina Bratt; Tucker, G. Richard (February 14, 2003). "Some Sociolinguistic Principles". Katika Labov, William. Sociolinguistics: The Essential Readings. Wiley-Blackwell. ku. 234–250. ISBN 0-631-22717-2.  Check date values in: |date= (help)
  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Matamshi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.