Lemuri
Fuvu la Mesopropithecus globiceps
Fuvu la Mesopropithecus globiceps
Uainishaji wa kisayansi
Domeni: Eukaryota (Viumbe walio na seli zenye kiini)
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Primates (Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Nusuoda: Strepsirrhini (Wanyama wanaofanana zaidi na lemuri)
Oda ya chini: Lemuriformes (Wanyama kama kima)
Familia ya juu: Lemuroidea (Lemuri)
Familia: Palaeopropithecidae
Jenasi: Mesopropithecus
Standing, 1905
Ngazi za chini

Spishi 3:

Mesopropithecus ni jenasi ya lemuri aliyewahi kuishi Madagaska; alikuwa mkubwa zaidi kuliko komba yeyote kati ya hawa walio hai leo.

Waligawanyika katika spishi tatu: M. dolichobrachion, M. globiceps na M. pithecoides.

Mesopropithecus pamoja na Palaeopropithecus, Archaeoindris, and Babakotia wapo katika familia ya wanyama jamii ya lemuri-slothi (Palaeopropithecidae).

Spishi zote tatu zilikuwa zinakula majani, matunda na mbegu, lakini uwiano ulikuwa tofauti.

M. pithecoides alikuwa hasa anakula majani, lakini pia alikuwa anakula matunda na mara kwa mara alikuwa akila mbegu.

M. globiceps alikuwa anakula mchanganyiko wa matunda na majani, pamoja na kiasi kikubwa cha mbegu kuliko M. pithecoides.

M. dolichobrachion pia alitumia mchanganyiko wa matunda na majani kwa kula, lakini uchambuzi wa meno yake unaonyesha kwamba ilikuwa zaidi mbegu kuliko aina nyingine yoyote.

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mesopropithecus kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.