Mgonjwa ni mtu aliyeingiliwa na maradhi.

Hii ni picha inayoonesha mgonjwa akiwa hospitali na wanajeshi wamemtembelea.
Mhindi huyu ana njaa, yaani ugonjwa wake umesababishwa na upungufu wa chakula.

Mgonjwa anapoumwa huonesha dalili mbalimbali za wazi, kwa mfano mgonjwa wa kichwa hushika kichwa. Kuna pia dalili nyingine za ndani ambazo ni muhimu zaidi kwa sababu zinadokeza chanzo cha ugonjwa ambacho ni muhimu kuwahi kupambana nacho.

Mgonjwa huteseka pale ambapo anapoumwa halafu hapewi huduma ya kwanza au hata kumwahisha hospitali. Ni muhimu kuzingatia kwamba kila mtu ana haki ya kuishi, tena vizuri, hivyo ana haki ya kutibiwa.

Pamoja na hayo, utu unadai kumpatia mgonjwa mahitaji yake mengine kwa mwili (chakula n.k.) na kwa nafsi (k.mf. pendo na faraja).

Dini mbalimbali zinaelekeza namna ya kumhudumia hadi mwisho. Kwa mfano Wakristo wa madhehebu mbalimbali wanamuombea na kumpatia sakramenti, zikiwemo kitubio, mpako wa wagonjwa na ekaristi.

Njia za maambukizi hariri

Baadhi ya maradhi husababishwa na virusi na bakteria.

Kuna njia mbalimbali za maambukizi ambazo ni:

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mgonjwa kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.